Kwa mujibu wa gazeti la Daily Independent, kanali hii imeanzishwa kwa lengo la kuelimisha jamii kubwa ya Waislamu nchini Nigeria. Kanali hii ilianza kurusha matangazo yake hewani katika Sikukuu ya Idul Adh'ha ambapo kulikuwa na vipindi vya kielimu na burudani.
Kanali hii ya televisheni itakuwa ikirusha matangazo ya Kiislamu kwa muda wa masaa 24 kwa siku.
Wakuu wa Nigeria wamesema wafuasi wa dini zote watapewa vibali vya kuanzisha kanali binafsi za televisheni.
699168