Halikadhalika hivi karibuni wakati wa Sala ya Idul Adha, magaidi waliushambulia kwa bomu Msikiti wa al Balili mjini Sana’a.
Kundi la kigaidi la ISIS au Daesh limedai kuhusika na hujuma hizo. Misikiti imekuwa ikilengwa na magaidi wa Daesh na pia ndege za kivita za Saudia zinazoendeleza hujuma dhidi ya Yemen.
Saudi Arabia ilianza kuishambulia Yemen tarehe 26 Machi mwaka huu kwa lengo la kuiondoa madarakani harakati ya Ansarullah. Mashambulizi hayo ya Saudia yameua Wayemen wasio na hatia zaidi ya 6,200 wengi wao wakiwa ni raia hasa wanawake, watoto wadogo na wazee. Saudia pia imedondosha mabomu katika misikiti, shule, viwanda na mahospitali katika maeneo mbalimbali ya Yemen.../mh