IQNA

Finland yazuia ujenzi wa msikiti unaofadhiliwa na utawala wa Bahrain

10:51 - December 21, 2017
Habari ID: 3471318
TEHRAN (IQNA)-Serikali ya Finland imekataa kutoa idhini ya ujenzi wa msikiti uliokuwa umepangwa kufadhiliwa na Bahrain katika mji mkuu wa nchi hiyo, Helsinki.

Taarifa zimesema wakuu wa mji wa Helsiniki wanakataa kuidhinisha ujenzi wa msikiti huo kwa sababu unafadhiliwa na utawala wa Bahrain unaoongozwa na ukoo wa Aal Khalifa.

Vyombo vya habari nchini Finland vimesema hali ya kisiasa nchini Bahrain na hatua ya utawala wa Aal Khalifa kukandamiza maandamano ya amani nchini humo ni kati ya sababu zilizopelekea kutopata kibali cha ujenzi msikiti huo.

Wasimamizi wa mradi huo wanasema msikiti huo ulikuwa unatazamiwa kuwa na nafasi za watu 2100 ikiwa ni pamoja na suhula za afya na michezo.

Tangu mwezi Februari 2011 hadi sasa, Bahrain inaendelea kushuhudia wimbi la malalamiko ya wananchi wanaotaka mageuzi ya kisiasa, kuweko utawala wa sheria, kufanyika uchaguzi huru na wa kidemokrasia na kuondolewa ubaguzi na upendeleo wa kimadhehebu na kikaumu nchini humo.

3464729

captcha