IQNA

Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran: Ulimwengu wa Kiislamu umtetee Sheikh Zakzaky

17:31 - December 20, 2019
Habari ID: 3472290
TEHRAN (IQNA) -Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa Tehran ameashiria matukio ya hivi karibuni katika nchi za Kiislamu na kusema kuwa, kuna ulazima kwa Waislamu kuwa macho mbele ya njama za maadui huku akitoa wito kwa Waislamu duniani kumtetea Sheikh Ibrahim Zakzaky wa Nigeria.

Ayatullah Mohammad Imami Kashani, katika hotuba zake za Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesema, waistikbari na mabeberu daima wanataka kutoa pigo kwa Waislamu na kuongeza kuwa: "Kundi la kigaidi la ISIS au Daesh lilianzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ili kwa njia hiyo waweze kukidhi maslahi yao (haramu)."

Ayatullah Imami Kashani ameendelea kusema kuwa, wasaliti wengi nchini Iraq ambao wanaungwa mkono na maadui wametumia vibaya maadamano ya wananchi wanaodai haki zao na kwa msingi huo wananchi wa Iraq wanapaswa kuwa waangalifu.

Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran aidha amekosoa muamala mbaya wa serikali ya Nigeria kwa Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo na kuongeza kuwa, ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kujitahidi kuhakikisha kuwa Sheikh Zakzaky anaachiliwa huru haraka. 

3865363

captcha