IQNA

Wakristo Misri wawatayarishia Waislamu Futari mwezi wa Ramadhani - Video

17:27 - May 15, 2020
Habari ID: 3472769
TEHRAN (IQNA) – Tokea mwaka 1975, Wakristo nchini Misri wamekuwa wakiwatayarishia Waislamu futari katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, futari hiyo hupewa jina la  'Dhifa ya Futari ya Umoja wa Kitaifa na huandaliwa na Wakristo katika maeneo mbali mbali ya Misri. Hata baada ya msukosuko ulioikumba Misri kutokana na mwamko na mapinduzi ya Januari 25 2011 bado dhifa hiyo ya futari imekuwa ikiendelea balo hata sasa imeimarika zaidi.

Wakristo wanakadiriwa kuwa asilimia 10 watu wote takribani milioni 98 katika nchi hiyo ya Kiislamu iliyo kaskazini mwa Afrika.

3898704

captcha