Kwa mujibu wa Baraza la Usalama wa Taifa na Wizara ya Afya, serikali imeruhusu misikiti na surau (kumbi za kidini) kufunguliwa maadamu shheria za kuzuia kuenea COVID-19 zitazingatiwa. Kati ya masharti yaliowekwa ni kuwataka waumini watawadhe nyumbani, wafike msikitini wakiwa na mazulia ya mikeka binafsi ya kuswalia, kuzingatia kanuni za kutokaribiana na kuvaa barakoa wakati wote wakiwa msikitini. Aidha misikiti inatakiwa kuwa na vifaa vya kupima kiwango cha joto mwilini na pia kuwapa waumini huduma ya kunawa mikono kwa kutumia dawa maalumu ya kuua viruzi na halikadhalika kusajili majini ya watu wote wanaofika msikitini kwa kutumia aplikesheni maalumu ijulikanayo kama MySejahtera au daftari maalumu.
Hadi sasa walioambukizwa COVID-19 nchini Malaysia ni 8,529 na waliopoteza maisha ni 121.