IQNA

Qarii wa Misri asoma Qur’ani akiwa amevaa barakoa + Video

13:04 - June 28, 2020
Habari ID: 3472906
TEHRAN (IQNA) – Qarii mashuhuri wa Qur’ani nchini Misri, Sheikh Abdul Fattah Taruti amesoma Qur’ani Tukufu akiwa amevaa barakoa.

Katika klipu ya video ambayo imeenezwa katika mitandao ya kijamii kupitia  chuo cha Darul Qur’an al Karim kinachofungamana na Kituo cha Kiislamu cha Hamburg, Ujerumani , qarii huyo wa mashuhuri anasoma Qur’ani Tukifi akiwa amevaa barakoa.

Klipu hiyo inamyonyesha akisoma aya za Qur’ani Tukufu za Surah Ar-Rum. Sheikh Taruti na baadhi ya hadhirina wanaonekana wakiwa wamevaa barakoa ikiwa ni katika kufuata kanuni zilizowekwa za kuzuia kuenea ugonjwa wa corona au COVID-19.

3907265

captcha