Mufti wa Uganda Sheikh Ramadhan Mubajje aliongoza Swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Kitaifa eneo la Old Kampala.
Amesema serikali itatumia kipindi hiki cha kupunguzwa utekelezwaji wa kanuni za kuzuia corona kuona ni vipi nyumba za ibada zitazingatia kanuni za kiaffya zilizowekwa. Sheikh Mubajje ametoa wito kwa Waislamu kuzingatia maelezo ya serikali kuhusiana na kukabiliana na corona. Naye Mufti Mkuu wa Uganda Sheikh Silimani Ndirangwa ametoa wito kwa serikali kuondoa marufu ya swala za jamaa.
Hadi sasa watu 7,218 wameambukizwa corona nchini Uganda ambapo waliofariki ni 71.