IQNA

Wapalestina waadhmisha miaka miongo mwili ya mwamko wa Intifadha ya Pili

20:30 - September 29, 2020
Habari ID: 3473213
TEHRAN (IQNA)- Jumatatu tarehe 28 Septemba, imesafidiana na kutimia miaka 20 tangu kulipotokea Intifadha ya Pili inayojulikana kama Intifadha ya al-Aqswa.

Hatua ya Ariel Sharon kiongozi wa wakati huo wa chama cha Likud na aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa utawala ghasibu wa Israel ya kuuvunjia heshima msikiti wa al-Aqswa, iliandaa uwanja wa kuanza Intifadha ya al-Aqswa tarehe 28 Septemba mwaka 2000. Katika Intifadha hiyo iliyochukua muda wa miaka 5, Wapalestina wapatao 4,412 waliuawa shahidi na wengine takribani 49,000 walijeruhiwa. Aidha Waisrael wapatao1,100 waliangamizwa huku mamia miongoni mwao wakijeruhiwa.

Intifadha ya al-Aqswa ilianza katika hali ambayo, utawala wa Kizayuni wa Israel ulikuwa umelazimika kuondoa majeshi yake kutoka kusini mwa Lebanon. Ukweli wa mambo ni kuwa, Israel ilifanya hujuma dhidi ya Msikiti wa al-Aqswa ili kufidia kushindwa kwake na muqawama wa Lebanon na kisha ukiliweka katika ajenda zake suala la kuanzisha vita dhidi ya Wapalestina. Nukta nyingine ni kuwa, Intifadha ya al-Aqswa ilianza katika mazingira ambayo, Mamlaka ya Ndani ya Palestina ilikuwa imeutambua rasmi utawala ghasibu wa Israel na mazungumzo ya mapatabno baina ya pande mbili yalikuwa yakiendelea.

Makubaliano ya Oslo baina ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina na utawala wa Kizayuni wa Israel yalitiwa saini 1993 ambapo kwa mtazamo wa Nafiz Azzam, mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina ni kuwa, baadhi waliyatambua makubaliano hayo kuwa yamebeba maana ya kufikia tamati muqawama na mapambano ya Palestina. Pamoja na hayo, moja ya matokeo muhimu ya Intifadha ya al-Aqswa yalikuwa ni kuimarika makundi ya muqawama huko Palestina.

Ukweli ni kuwa, Intifadha ya al-Aqswa sambamba na kuthibitisha kutokuwa na natija mwenendo wa mapatano na Israel, imeonyesha kuwa, mpambano na muqawama ni utendaji uliokubaliwa na wananchi wa Palestina. Katika uwanja huo, Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS ilifanikiwa kuibuka na ushindi katika uchaguzi wa Bunge wa mwaka 2005 na kisha ikaunda serikali.

Baada ya kupita miongo miwili tangu ilipoanza Intifadha ya al-Aqswa, hali ya Palestina ipo kwa namna ambayo kuna uwezekano wa kuanza Intifadha mpya. Gazeti la al-Qus al-Arabi limeandika katika moja ya ripoti zake kuhusiana na kadhia hii kwamba: Utawala wa Kizayuni wa Israel ungali unaendelea na ujenzi wake wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi sambamba na ukaliaji mabavu ardhi ya Palestina.

3472665

captcha