Kwa mujibu wa taarifa, Idara ya Masuala ya Al-Masjid an-Nabawi imesambaza picha za Waislamu kutoka nje ya Saudia ambao wamefika Madina na kuutembelea msikiti huo mtakatifu.
Wote wanaofika katika Al-Masjid an-Nabawi wanatakiwa kuzingatia kanuni za afya ili kuzuia kuenea ugonjwa wa corona.
Kwa mujibu wa sheria zilizowekwa Waislamu 160-170 wanaruhusiwa kutembelea Msikiti wa Mtume SAW. Kwa ujumla msikiti huo unatembelewa na Waumini wasiozidi 5,00 kwa siku. Kuanzia Novemba 1 mwaka huu raia wa kigeni waliruhusiwa kuingia Saudia kwa ajili ya kutekeleza ibada ya Umrah na kutembelea Al-Masjid an-Nabawi.