IQNA

Hizbullah yamsifu waziri mkuu wa zamani wa Sudan Sadqi al-Mahdi

17:02 - November 27, 2020
Habari ID: 3473399
TEHRAN (IQNA) – Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetuma salamu za rambi rambi kufuatia kuaga dunia waziri mkuu wa zamani wa Sudan Sadiq al-Mahdi na kumtaja kuwa muungaji mkono mkubwa wa Palestina aliyepinga uanzishwaji uhusiano wowote na utawala wa Kizayuni wa Israel.

Katika taarifa Alhamisi, Hizbullah immemtaja Sadiq al-Mahdi kuwa mwanasiasa aliyeheshimika kutokana na msimamo wake wa kupambamna na kupinga mabeberu wa kimataifa.

Al-Mahadi alifariki juzi baada ya kuambukizwa corona kwa muda wa iki tatu. Al-Mahdi, 84, alikuwa waziri mkuu wa mwisho kuchaguliwa kidemokrasia na alipinduliwa mwaka 1989 katika mapinduzi ya kijeshi yaliyomleta madarakani rais wa zamani Omar al-Bashir ambaye naye pia alipinduliwa na jeshi mwaka 2019.

Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, nayo pia imetuma salamu za rambi rambi kufuatia kuga dunia al-Mhadi na kumtaja kuwa muungaji mkono wa haki za Wapalestina.

3473236

captcha