IQNA

Malaysia: Chanjo ya COVID-19 haihitaji cheti cha ‘Halal’

23:16 - December 09, 2020
Habari ID: 3473439
TEHRAN (IQNA) – Chanjo ya COVID-19 au corona inayosuburiwa kwa hamu, haina haja ya kupata cheti cha ‘Halal’ kabla ya kutumika nchini Malaysia, amesema mkurugenzi mkuu wa Wizara ya Afya nchini humo Daktari Noor Hisham Abdullah.

Kauli hiyo ya afisa huyo wa afya Malaysia inaondoa wasiwasi uliopi miongoni mwa Waislamu kuwa yamkini chanjo ya COVID-19 ina mada ambazo zimeharamishwa katika Uislamu.

Alhamisi iliyopita, Baraza la Kitaifa la Masuala ya Kiislamu lilikutana kujadili iwapo Waislamu wanaweza kupata chanjo ya COVID-19. Waziri wa Masuala ya Kidini Malaysia, Zulkifli Mohammad Al Bakri alisema uamuzi wa mwisho utatangazwa baada ya kuwasilishw akwa mfalme, ambaye husimamia masuala ya kidini nchini humo.

Shirika la dawa la Malaysia, Pharmaniaga, linapanga kujenga kiwanda cha kwanza cha chanjo halali mwaka 2022. Malaysia tayari imeshatia saini mikataba na mashirika ya  COVAX na Pfizer kwa ajili ya kupata chanjo ya COVID-19 kwa ajili ya asilimia 20 ya wale ambao ni dharura kupata chanjo.

3473361

captcha