Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema katika ujumbe wake kupitia Twitter na ambao ameutuma kwa lugha ya Kiingereza kwamba, anawatakia kheri Wakristo wa Iran na duniani kiujumla katika sherehe za za Krismasi za kukumbuka kuzaliwa Nabii Isa mwana wa Maryam AS.
Katika ujumbe huo, Ayatullah Khamenei amesema: "ninatoa mkono wa baraka kwa Wakristo na Waislamu kote duniani na hasa raia wenzangu wa Iran wa dini ya Kikristo kwa mnasaba wa maadhimisho ya siku ya kuzaliwa Nabii Isa Masih- Amani ya Mwenyezi Mungu Iwe Juu Yake-."
Wakristo duniani, jana Ijumaa waliadhimisha sikukuu ya Karismasi wanayoinasibisha na siku ya kuzaliwa Nabii Isa mwana wa Maryam AS, sherehe ambazo hufanyika tarehe 25 Disemba kila mwaka.