IQNA

Al Azhar: Chanjo ya COVID-19 haibatilishi saumu

19:57 - March 07, 2021
Habari ID: 3473713
TEHRAN (IQNA) – Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar kimetangaza kuwa kudungwa chanjo ya Corona au COVID-19 haitabatilisha Saumu ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Kwa mujibu wa tovuti ya albayan, Kituo cha Kimataifa Fatuwa cha Al Azhar, kimechapisha taarifa katika ukurasa wake wa Facebook na kusema kwa kuzingatia kuwa chanjo ya Corona haiingizwe mwilini kupitia mdomo au pua basi haibatilishi Saumu.

Aidha kituo hicho kimesema chanjo ya Corona haitambuliwa kuwa ni aina ya chakula au kinywaji na inatumika kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa hivyo haibatilishi Saumu.

Pamoja na hayo, Kituo cha Fatwa cha Al Azhar kimependekeza kuwa, iwapo Mwislamu atadungwa chanjo ya Corona katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani basi adungwe baada ya Futari. Hii ni kwa sababu yamkini mwenye kudungwa chanjo ya Corona akahitajia lishe ya haraka kutokana na athari za chanjo hiyo.

فتوى لقاح كورونا

Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unatazamiwa kuanza Aprili 12 2021 kwa kutegemea mwezi mwandamo.

3958029

captcha