IQNA

Waislamu waukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani duniani

21:25 - April 13, 2021
Habari ID: 3473808
TEHRAN (IQNA)- Waislamu katika baadhi ya nchi wameanza Saumu ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani mnamo Aprili 13 baada ya mwezo mwandamo kuonekana Jumatatu katika baadhi ya maeneo ya dunia.

Nchi zilizotangaza leo kuwa siku ya kwanza ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni pamoja na Malaysia, Indonesia, Australia, Japan na baadhi ya nchi za Ghuba ya Uajemi.  Katika nchi hizo Waislamu wameshiriki katika Sala ya Tarawih kwa kuzingatia kanuni za kiafya za kuzuia kuenea COVID-19.

Nchi zingine kama vile Iraq, Iran, Tanzania na Kenya zimetangaza rasmi kuwa Aprili 14 ni siku ya kwanza ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

 

Kishikizo: ramadhani dunia covid 19
captcha