IQNA

Raia wa Mauritania ashinda mashindano ya Adhana Senegal + Video

22:27 - May 26, 2021
Habari ID: 3473949
TEHRAN (IQNA) – Mashidano ya Adhana yamefanyika hivi karibuni nchini Senegal na kushirikisha nchi tatu za Afrika Magharibi.

Mashindano hayo yalipewa jina la Bilal ibn Rabah (RA), Sahaba wa Mtume Muhammad SAW ambaye alikuwa Muadhini wa kwanza katika Uislamu.

Mashindano hayo yalikuwa na washiriki 250 kutoka Senegal, Mauritani na Gambia.

Mshindi alikuwa, Muhammad Abdul Ja , mvulana mwenye umri wa miaka 12 kutoka Mauritania.

Hii hapa ni klipu ya mashindano hayo.

3973628

captcha