IQNA

Imam Khomeini ni wa Waislamu na wasiokuwa Waislamu

13:28 - June 16, 2021
Habari ID: 3474011
TEHRAN (IQNA)- Imam Khomeini-Mwenyezi Mungu Amrehemu- ni shakhsia ambaye ambaye hakuwa tu ni wa Waislamu bali pia alikuwa ni wa wasio kuwa Waislamu nchini Iran na kote duniani.

Haya ni kwa mujibu wa Mar Narsai Benjamin, Askofu wa Kanisa la Asyria nchini Iran wakati alipohutubu katika kongamano la Kimataifa la 'Imam Khomeini na Ulimwengu wa Kisasa' lililofanyika Tehran Juni 3.

Kongamano hilo lilifanyika katika Haram Takatifu ya Imam Khomeini MA kusini mwa Tehran.

Amesema Imam Khomeini alikuwa anapenda na watu wote na alikuwa ni muokozi aliyetumwa na Mwenyezi Mungu kulikomboa taifa la Iran.

3474940

captcha