IQNA

Qarii maarufu wa Misri Abdul Halim aaga dunia

20:10 - June 25, 2021
Habari ID: 3474042
TEHRAN (IQNA)- Qarii maarufu wa Misri Sheikh Muhammad Abdul Halim ameaga dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa taarifa, qarii huyo maarufu wa Misri alipoteza maisha Jumatano kutokana na maradhi sugu ya muda mrefu.

Sheikh Abdul Halim amezikwa katika mji wa Talkha mkoani Dakahlia kaskazini mashariki mwa Cairo. Watu wa Misri wamemuomboleza katika mitandao ya kijamii ambapo wamemuombea maghufira huku wakisambaza klipu za qiraa yake.

3979740

Kishikizo: abdul halim qarii misri
captcha