IQNA

Rais wa Iran ahutubu katika Msikiti Mkuu wa Moscow, Russia

19:13 - January 21, 2022
Habari ID: 3474831
TEHRAN (IQNA)- Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu amesema mbele ya Waislamu wa Msikiti Mkuu wa Moscow, mji mkuu wa Russia kwamba, Misikiti ni nyumba za Mwenyezi Mungu ardhini na inamlea vizuri Muislamu na jamii yake.

Ameongeza kuwa, mbali na Misikiti kuijenga vizuri nafsi ya mwanadamu na kuimarisha uhusiano wake na Mwenyezi Mungu, nyumba hizo za Allah zinajenga na kuimarisha pia uhusiano mzuri wa kijamii wa Waislamu.

Rais Ebrahim Raisi amekwenda katika Msikiti Mkuu wa Moscow kwa mwaliko ya Mufti Mkuu wa Russia, Sheikh Rawil Gaynetdin na ameonana kwa karibu na Waislamu na kuzungumza nao.

Amesema, kuenea ufisadi na maadili maovu katika kila kona ya dunia leo hii ni ushahidi thabiti kwamba mwanadamu leo amemsahau Muumba wake. Amesema, miaka 70 imepita wananchi wa Palestina wanadhulumiwa na Wazayuni watenda jinai na zaidi ya miaka 20 wananchi wa Afghanistan waliishi chini ya uvamizi, ukatili na mauaji na hayo ni matunda ya siasa zisizo na maadili wala umaanawi.

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amegusia pia umuhimu wa Waislamu kushikamana vilivyo na mafundisho sahihi ya dini yao na kujiimarisha kiroho na kimaanawi akisisitiza kuwa, jinai zinazofanywa na magenge ya wakufurishaji katika nchi za Syria, Iraq, Afghanistan na Yemen tena kwa jina la Uislamu ni mambo ambayo hayana uhusiano wowote wa dini tukufu ya Uislamu bali ni njama za Markeani na Wazayuni ndizo zonazochochea na kuendesha jinai hizo.

Vile vile amesema, moja ya kazi muhimu za Misikiti katika Umma wa Kiislamu ni kuwaamsha Waislamu na kuzuia kuenea fikra za ukufurishaji na kwamba siri ya mtu kuwa Muislamu wa kweli ni kuimarisha nafsi yake na kuwatendea mema wengine.

Ikumbukwe kuwa,

Sayyid Ebrahim Raisi, Rais wa Jamhuri ya Kiisalmu ya Iran siku ya Jumatano alikutana na kufanya mazungumzo na Rais Vladimir Putin wa Russia mjini Moscow ambapo pande mbili zimejadili masuala ya kieneo na kimataifa.

Katika mazungumzo hayo, Rais Raisi ameashiria nafasi muhimu na yenye taathira ya Russia na Iran katika eneo na dunia na kusema: "Ufahamu wa pamoja wa nchi mbili kuhusu masuala ya kieneo na kimataifa ni msingi wa ushirikiano wa pamoja. Uhusiano wa Russia na Iran uko katika mkondo wa pamoja wa kimkakati."

Aidha Raisi amesema kipaumbele katika sera za kigeni za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kuwa na maingiliano mema na nchi jirani na waitifaki na kuongeza kuwa, "kuimarishwa ushirikiano wa Iran na Russia kutapelekea kuboreka uchumi wa nchi mbili na pia kuimarika kiwango cha usalama wa kieneo na dunia nzima."

Kwa upande wake, Rais Vladimir Putin wa Russia amesema hivi sasa kunatekelezwa miradi mikubwa ya maendeleo baina ya nchi mbili na kuongezwa kuwa Iran na Russia zinaendeleza ushirikiano katika nyanja mbali mbali. Ameendelea kusema: "Katika uga wa kimataifa, tuna ushirikiano wa karibu. Kwa jitihada za nchi hizi mbili, tumeweza kuisaidia Syria kukabiliana na magaidi wa kimataifa."

3477467

captcha