IQNA

Ubelgiji, ardhi marufuku kwa watenda jinai za kivita wa Israel

11:43 - January 29, 2009
Habari ID: 1737418
Utawala haramu wa Israel umewakataza askari na viongozi wake rasmi kufanya safari nchini Ubelgiji kwa woga wa kukamatwa na kufikishwa mahakamani kutokana na mashambulizi ya utawala huo katika Ukanda wa Gaza na mauaji ya kinyama yaliyofanywa dhidi ya raia wa eneo hilo la Palestina.
Maafisa wa jeshi la Israel ni miongoni mwa watu waliozuiwa kufanya safari katika nchi kadhaa ikiwemo Ubelgiji kutokana na jinai zilizofanyika huko Gaza.
Habari zinasema kuwa mashtaka yaliyowasilishwa mahakamani mwaka 2002 dhidi ya Waziri Mkuu wa zamani wa Israel Ariel Sharon kwa kutenda mauaji dhidi ya Wapalestina yamepata nguvu zaidi kwa kuunganishwa na kesi ya sasa na mashambulizi ya utawala huo wa kigaidi katika Ukanda wa Gaza.
Waziri wa Mambo ya Nje wa utawala wa Kizayuni wa Israel Tzipi Livni pia amevunja safari yake nchini Ubelgiji baada ya ukurasa mmoja wa intaneti kuandika kuwa, kiongozi huyo anasakwa kwa tuhuma za kutenda jinai za kivita katika Ukanda wa Gaza. 355810

captcha