IQNA

Onyo la kamati ya uandaaji wa tamasha la Quds Tukufu kuhusu njama za utawala wa Kizayuni dhidi ya mji huo

10:26 - February 28, 2009
Habari ID: 1749218
Kamati inayoandaa tamasha la 'Quds Tukufu: Mji Mkuu wa Kiutamaduni wa Waarabu' imetoa taarifa ikilaani siasa za utawala haramu wa Israel za kuharibu maeneo matakatifu ya Wapalestina na za kuuteka mji mtukufu wa Quds.
Huku ikiashiria njama za utawala huo za kuwafukuza Wapalestina kutoka katika ardhi na makazi yao katika mji huo, kamati hiyo imesema kuwa utawala huo una lengo la kuwafukuza Wapalestina wapatao 1500 kutoka katika eneo la Bustan karibu na Msikiti wa al-Aqsa na kuharibu nyuma zao zipatazo 88.
taarifa hiyo Imesisitiza kwamba, njama hizo zina lengo la kuharibu kabisa muundo wa mji huo mtukufu na kuufanya kuwa na utambulisho wa Kiyahudi. Taarifa ya kamati hiyo imeendelea kusema kuwa, wakazi wa Kipalestina wa mji huo ambao wametengwa na wenzao na ukuta wa kibaguzi uliojengwa hivi karibuni na Wazayuni katika eneo hilo, kwa hakika wamezingirwa na kulazimishwa kuishi kama wafungwa.
Imesema, Wapalestina hao wamenyimwa kabisa uwezekano wa kuwa na mawasiliano na ulimwengu wa nje. Hata hivyo, taarifa hiyo inasisitiza kwamba jambo hilo halipasi kuwafanya Wapalestina kuendelea kunyimwa haki zao za kimsingi, ikiwemo ya kurejea katika ardhi zao za jadi. 369793
captcha