IQNA

Makka, mwenyeji wa kikao cha kimataifa cha 'Ulimwengu wa Kiislamu; Matatizo na Utatuzi"

11:54 - April 21, 2011
Habari ID: 2109506
Kikao cha kimataifa cha 'Ulimwengu wa Kiislamu; Matatizo na Utatuzi' kimepangwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu kufanyika katika mji mtakatifu wa Makka tokea tarehe 24 hadi 26 Julai mwaka huu.
Kikao hicho ambacho kitahudhuriwa na wanazuoni na wasomi wa Kiislamu kutoka nchi mbalimbali za dunia kitajadili hali ya hivi sasa ya Waislamu na matatizo ya ulimwengu wa Kiislamu pamoja na njia za kuyatatua. Akizungumzia suala hilo Abdallah bin Abdul Muhsin at-Turki Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu ameashiria umuhimu wa kufanyika kikao kama hicho na kuongeza kuwa jumuiya hiyo imekuwa ikifuatilia kwa karibu matatizo ya nchi za Kiislamu na kujaribu kunufaika na fikra za wasomi na wanafikra wa Kiislamu katika kuyatatua. 777614
captcha