IQNA

Shirika la ndege la Air France lamfukuza kazi mwanamke wa Kiislamu mvaa hijabu

12:07 - June 25, 2011
Habari ID: 2143775
Shirika la ndege la Air France tawi la Washington limemfukuza kazi mfanyakazi wake wa kike wa Kiislamu kutokana na uamuzi wake wa kuendelea kuvaa hijabu.
Kwa mujibu wa tovuti ya Lexpress, habari hiyo imefichuliwa na Halmashauri ya Uhusiano wa Marekani na Uislamu CAIR na kwamba uchunguzi kuhusu jambo hilo ungali unaendelea. Halmashauri hiyo inasema kuwa, baada ya kukabiliwa na mashinikizo ya Waislamu, mkuu wa shirika la Air France nchini Ufaransa ameahidi kuchunguza tukio hilo la kusikitisha na la chuki dhidi ya Uislamu.
CAIR wakati huohuo imelitaka shirika hilo limrejeshe kazini mwanamke huyo wa Kiislamu haraka iwezekanavyo.
Hadi sasa hakuna habari kamili ambazo zimetolewa kuhusiana na shughuli hasa ya mwanamke huyo katika shirika hilo. 814166
captcha