IQNA

Hizbullah ya Lebanon yawapongeza Waislamu wa Tunisia kwa kushinda uchaguzi

12:54 - October 27, 2011
Habari ID: 2212715
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon Hizbullah imetoa taarifa ikiwapongeza Waislamu wa Tunisia kutokana na ushindi mkubwa waliopata katika uchaguzi wa hivi karibuni nchini humo.
Imewashukuru pia wananchi wote wa nchi hiyo kwa kushiriki kwa wingi katika uchaguzi huo wa kwanza wa kidemokrasia. Imesema kwa kushiriki kwa wingi katika uchaguzi huo wa bunge ambalo litabuni katiba mpya ya Tunisia, wananchi hao wamepiga hatua muhimu katika kujiainishia mustakbali wao.
Taarifa ya Hizbullah imesema kwamba ushiriki mkubwa wa Watunisia katika uchaguzi wa hivi karibuni kwa mara nyingine tena umethibitisha wazi kwamba kila taifa linalotaka kuishi kwa utukufu na heshima kamwe haliwezi kuacha mapambano ya kufikia lengo hilo na kuwa litaendelea kupigania kwa uwezo na irada yake yote mustakbali na historia yake.
Taarifa ya Hizbullah imeyataka makundi ya Kiislamu ya Tunisia kufanya kila liwezekanalo ili kutekeleza matakwa ya mashahidi na wananchi wa nchi hiyo ambao wamejitolea mhanga kwa shabaha ya kulinda kujitawala, uadilifu na utukufu wa nchi hiyo. 888140
captcha