Akizungumza Jumamosi, Rais Rouhani amesema Sala ya Idul Fitri itaswaliwa katika maeneo mbali mbali kote nchini.
Hatahivyho amesema kinyume na ilivyo ada Sala ya Idi haitaswaliwa katika viwanja vikubwa vya miji bali itaswaliwa katika misikiti au vituo vya kidini vya mitaa mbali mbali.
Rais Hassan Rouhani ameyasema hayo wakati alipohutubu katika Makao Makuu ya Kupambana na COVID-19 ambapo amesema maadhimisho ya Siku ya Quds yatafanyika katika maeneo ambayo kirusi cha COVID-19 si tishio. Amesema Siku ya Kimataifa Quds itaadhimishwa ndani ya maeneo ya Swala ya Ijumaa na kwamba hakutakuwa na matembezi ya kawaida. Aidha amesema kuwa katika mji mkuu Tehran, wananchi watajitokeza mitaani wakiwa ndani ya magari yao chini ya usimamizi wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC).
Siku ya Kimataifa ya Quds huadhimishwa katika Ijumaa ya Mwisho ya Mwezti Mtukufu wa Ramadhani,.
Mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu hayati Imam Khomeini (Mwenyezi Mungu amrehemu) ndiye aliyeipa siku hiyo ya Ijumaa ya mwisho ya mwezi Ramadhani jina la Siku ya Kimataifa ya Quds kwa shabaha ya kuakisi dhulma ya kihistoria inayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watu wanaoendelea kudhulumiwa na kukandamizwa wa Palestina na ardhi yao takatifu. Tokea ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran mwaka 1979, Siku ya Kimataifa ya Quds imekuwa ikiadhimishwa kupitia maandamano na makongamano kote duniani.