Zaidi ya wanachuo 100 kutoka vitivo mbali mbali vya chuo hicho walishiriki katika mashindano hayo ambapo Hamza Abubakr Swaleh wa Tanzania, ambaye anasoma katika Kitivo cha Qur’ani, aliibuka mshindi.
Nafasi ya pili ilichukuliwa na Abdullah Bassam wa Lebanon huku Watun Buniako wa Kosovo. Mashindano hayo yaliandaliwa na Kitivo cha Qur’ani cha Chuo Kikuu cha Al Qasimia.
Mashindano hayo yanalenga kutambua vipaji vya Qur’ani miongoni mwa wanachuo sambamba na kuwahimiza kuhifadhi na kusoma Qur’ani. Mashindano hayo yalifanyika kwa njia ya video kutokana na vizingiti vilivyowekwa baada ya kuibuka ugonjwa wa corona.