IQNA

Kiongozi wa Kuwait aaga dunia, televisheni yarusha hewani qiraa ya Qur’ani Tukufu

21:01 - September 29, 2020
Habari ID: 3473215
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi wa Kuwait Emir Sheikh Sabah Al Ahmad Al Sabah amefariki dunia na punde baada ya hilo kubainika, televisheni ya nchi hiyo ilikatiza matangazo ya kawaida na kuanza kurusha hewani qiraa ya Qur’ani Tukufu.

Al Sabah ambaye atakumbukwa kwa juhudi za kidiplomasia za kupigia debe uhusiano wa karibu na Iraq baada ya vita vya Ghuba ya Uajemi vya mwaka 1990, wakati akiwa waziri wa mambo ya nje,  pamoja na kutafuta suluhu katika mizozo mingine ya kikanda, amekufa leo Jumanne akiwa na umri wa miaka 91.

Ukanda wa Asia Magharibi au mashariki ya kati, Sheikh Sabah alisifika kwa juhudi zake za kuweka mbele diplomasia ili kusuluhisha mzozo kati ya Qatar na mataifa mengine ya Kiarabu.

Al Sabah aliingia madarakani mwaka 2006, baada ya bunge kupiga kura ya kumuondoa mamlakani mtangulizi wake Sheikh Saad Al Abdullah Al Sabah, siku tisa tu katika utawala wake. Nafasi yake inatarajiwa kujazwa na kaka yake, mfalme Sheikh Nawaf Al Ahmad Al Sabah mwenye umri wa miaka 83.

3926288/

Kishikizo: kuwait emir
captcha