IQNA

Wanajeshi tisa wa Australia wajiua baada ya ‘Ripoti ya Jinai za Kivita Afghanistan’

21:36 - November 23, 2020
Habari ID: 3473387
TEHRAN (IQNA) – Wanajeshi tisa wa Australia wamejiua katika kipindi cha wiki tatu baada ya ripoti kufichua jinai zilizotendwa na Kikosi cha SAS cha Jeshi la Australia nchini Afghanistan.

Taarifa za siri zimebaini kuwa baadhi ya wanajeshi wa Australia waliwaua raia wakiwemo watoto ambao hawakuwa na silaha nchini Afghanistan.

Baada ya kufichuliwa kasfha hiyo, wanajeshi tisa wamejiua hivi karibuni na miongoni mwa waliojiua ni mwanamke mmoja na wanaume nane.

Gazeti la The Advertiser limesema walijiua  baada ya klipu ya kushtua ya video kuonyesha mwanajeshi wa Australia akimuua raia wa Afghanistan.

Akiwasilisha muhtasari wa ripoti ya uchunguzi wa miaka minne mbele ya waandishi wa habari mjini Canberra hivi karibuni, Mkuu wa Jeshi la Australia Angus Campbell alisema kikosi maalum cha jeshi la Australia kilihusika na mauaji hayo dhidi ya wafungwa, wakulima na raia wa kawaida.

Jenerali Campbell alisema kuna rikodi za kutia aibu kama vile mwanajeshi kumuuwa mfungwa ili tu kupata ladha ya kumuuwa mtu wa kwanza, tendo ambalo kijeshi huitwa "kumwaga damu", na kisha baada ya mauaji kama hayo, wanajeshi walikuwa wakipandikiza silaha na redio ili kutunga madai ya uongo kwamba wahanga wao walikuwa maadui waliouawa kwenye mapambano.

Wanajeshi  hao wa Australia walikuwa waliwa nchini Afghanistan chini ya kikosi cha kimatiafa cha ISAF ambacho kinasimamiwa  na muungano wa kijeshi wa nchi za Magharibi NATO chini ya uongozi wa Marekani. 

Hayo yanajiri wakati ambao Majaji waandamizi katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wameamuru uchunguzi uanze kuhusu jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu ambazo zinaripotiwa kufanywa na askari wa Marekani nchini Afghanistan. Afghanistan ilivamiwa

na Marekani pamoja na waitifaki wake mwaka 2001 kwa kisingizio cha kukabiliana na ugaidi lakini si tu kuwa ugaidi haujapungua bali hata umeongezeka huku nchi hiyo ikishuhudia mashambulia ya magaidi karibu kila siku.

3473206

captcha