IQNA

Eneo la Nabi Musa, Jericho, Palestina inayokaliwa kwa mabavu

TEHRAN (IQNA)- Nabi Musa ni eneo ambalo liko kilomita nane kusini mwa Jericho (Ariha) katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa Israel na inaaminika kuwa hapo ndipo lililo kaburi la Nabii Musa-Amani ya Mwenyezi Mungu Iwe Juu Yake.

Jengo la Nabi Musa lilijengwa na mtawala wa Quds (Jeruslam) Salah al-Din Yusuf ibn Ayyub, kati ya karne 1138 na 1193 Miladia na ni kati ya maeneo matakatifu Palestina. Jengo hilo lenye ukubwa wa mita mraba 4500 ni nembo ya sanaa katika usanifu majengo wa Kiislamu.

 
 
Kishikizo: Nabi Musa ، palestina ، ariha ، jericho
Habari zinazohusiana