IQNA

Baraza Kuu la UN lapitisha aazimio dhidi ya Israel

20:10 - December 02, 2021
Habari ID: 3474630
TEHRAN (IQNA)- Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine tena limetaka kuondoka kikamilifu utawala ghasibu wa Israel katika Miinuko ya Golan inayokaliwa kwa mabavu na utawala huo.

Katika azimio ambao limepitishwa leo,  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeeleza kuwa, uamuzi uliochukuliwa na  Israel Disemba 14 mwaka 1981 wa kulazimisha sheria na kuamua kuikalia kwa mabavu Miinuko ya Golan huko Syria ni batili, usio na itibari na kinyume cha sheria. 

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limesema:"Kama ambavyo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilivyosisitiza katika azimio nambari 497 la mwaka 1981, Israel inapaswa kukomesha hatua zake na kuondoka kikamilifu katika eneo linalokaliwa kwa mabavu la Miinuko ya Golan tarehe 4 Juni mwaka 1967."

Nchi 94 wanachama wa Umoja wa Mataifa zimepiga kura ya ndiyo kwa azimio hilo la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Mwakilishi wa kudumu wa Syria katika Umoja wa Mataifa Bassam Sabbagh amehutubia kikao hicho cha Baraza Kuu la UN na kusema mwenendo wa sasa wa Umoja wa Mataifa wa kutotekeleza maazimio yake unaushajiisha utawala ghasibu wa Israel kuendeleza uvamizi na ukanzamizaji dhidi ya raia wa Syria katika eneo linalokaliwa kwa mabavu la Golan.

4017906

 

 

captcha