Mashindano hayo yaliyopewa jina la Zawadi ya Qur’ani Tukufu ya Hessa bin Muhammad yanatazamiwa kuendelea hadi Machi 10. Hii ni duru ya tisa ya mashindano hayo.
Kwa mujibu wa taarifa, mashindano hayo yameandaliwa na Taasisi ya Sultan bin Khalifa Al Nahyan kwa ushirikiano na Wizara ya Elimu na Idara ya Wakfu UAE.
Jumla ya wasichana 130 wanashiriki katika mashindano hayo ya kuhifadhi Qur’ani Tukufu katika kategoria 11.