TEHRAN (IQNA)- Lango la Qur'ani (Darvazeh-e-Qur'an) ni lango la kihistoria latika mji wa Shiraz kusini mwa Iran na moja ya vivutio vikuu vya kitalii katika mji huo.
Juu ya lango hilo kuna misahafu miwili ambayo imewekwa hapo kwa nia ya kuwabariki wanaoingia mjini humo na kwa ajili ya safari njema kwa wanaoondoka mjini humo.