IQNA

Mapambano dhidi ya utawala haramu wa Israel

Oman haitaanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel

21:37 - May 28, 2022
Habari ID: 3475308
TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman siku ya Jumamosi alitangaza kuwa nchi yake haitaanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel huku akitoa kutoa wito wa kutatuliwa kwa haki suala la Palestina.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Badr al-Busaidi ameliambia gazeti la Ufaransa la Le Figaro kuwa nchi yake ni nchi ya kwanza ya Kiarabu kwenye Ghuba ya Uajemi kuunga mkono amani Palestina tangu Makubaliano ya Camp David ya 1979.

Amesisitiza kuwa, Muscat haitajiunga na 'Makubaliano ya Abraham' ya kurejesha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa sababu inafadhilisha mipango mipango iliyopo ya kuwaunga mkono wananchi wa Palestina.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman alisema: "Mafanikio yoyote katika Makubaliano ya Abaraham ni lazima yalete suluhisho la mwisho, la kudumu na la haki kwa suala la Palestina kwa msingi wa suluhisho la serikali mbili."

Kauli hiyo ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman imekuja baada Olivia Benjamin, mkuu wa idara Mashariki ya Kati (Asia Magharibi) ya wizara ya mambo ya nje ya utawala haramu wa Israel hivi karibuni kudai kuwa Oman inaweza kuwa nchi inayofuata kurejesha uhusiano na utawala huo ghasibu.

UAE na Bahrain zilitia saini makubaliano ya amani na Israel mnamo Septemba 15, 2020, ikifuatiwa na Sudan na makubaliano ya kuhalalisha Oktoba 23, 2020, ikifuatiwa na Moroko mnamo Desemba 10, 2020, kwa msaada wa Amerika na rais wa zamani. , Donald Trump makubaliano.

Mwaka 2020 Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati), Bahrain, Sudan na Morocco ziliwasaliti Waislamu na Wapalestina kwa kutangaza uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel. Mapatano hayo yalifikiwa kwa himaya ya mtawala wa wakati huo wa Marekani Donald Trump na hivyo kuzifanya nchi hizo kujiunga na Misri na Jordan ambazo ndizo zilizokuwa nchi za kwanza za Kiarabu kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala bandia wa Israel.

4060271

captcha