IQNA

Aya za Machipuo/ 2

Ustadh Abdul Basit akisoma aya ya Qur'ani Tukufu kuhusu Mvua (+Video)

TEHRAN (IQNA) - Wakati Wairani na mataifa mengine kadhaa wakisherehekea siku kuu ya Nowruz, kuashiria mwanzo wa majira ya machipuo, ni wakati muafaka wa kuashiria aya za Qur'ani Tukufu kuhusu kuhuishwa ardhi katika majira ya kuchipua baada ya msimu wa majira ya baridi kali. Kwa hakika machipuo nidalili za rehema na uwezo wa Mwenyezi Mungu.

Hapa chini tunamsikiza qarii maarufu wa Misri Sheikh Abdul Basit Abdul Samad akisoma aya ya 21 ya Sura Az-Zumar na ni moja ya aya   ambamo Mungu anaangazia jinsi maji yatokayo angani yanavyobadilisha uso wa dunia.

 

 

 

 

"Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu ameteremsha maji kutoka mbinguni. Kisha akayapitisha kwenye chemchem katika ardhi, kisha kwa maji hayo akatoa mimea yenye rangi mbali mbali? Kisha hunyauka ukaiona imekuwa kimanjano, na kisha huifanya mapepe. Bila ya shaka katika hayo upo ukumbusho kwa wenye akili. "