
Njia hiyo inapendekezwa kuwa njia kutoka India hadi Ulaya kupitia Umoja wa Falme za Kiarabu, Saudi Arabia, Palestina iliyokaliwa na utawalahuo katili wa Israel na Ugiriki.
Kongamano maalum la 64 la Jukwaa la Kimkakati la Vyombo vya Habari na Mitandao ya Kijamii lilifanyika katika Shirika la Kimataifa la Habari za Qur'an (IQNA) huko Tehran Jumatano.
Lilihudhuriwa na watu wa vyombo vya habari, watafiti, na wanafunzi wa vyuo vikuu, lilikuwa na mijadala juu ya shughuli za vyombo vya habari kuhusu IMEC.
Hamid Reza Hosseini Dana, mkuu wa jukwaa hilo na katibu wa kisayansi wa kongamano hilo, alikuwa miongoni mwa wazungumzaji.
Alisema moja ya mijadala katika mashindano ya kiuchumi ya sasa na ya baadaye duniani ni juu ya njia kama vile Njia ya Kaskazini-Kusini, Njia ya Kati, na Njia ya Caucasus.
"Karibuni, wakati wa mkutano wa G20, njia iitwayo IMEC ilitangazwa. Njia hii, ikihusisha India kama mshiriki muhimu, inapanga kusafirisha bidhaa, huduma, hidrojeni ya kioevu, nishati, na umeme kutoka nchi za kusini mwa Ghuba ya Uajemi kupitia UAE, Oman, Saudi Arabia, na Jordan hadi kwa utawala wa Kizayuni na Bandari ya Haifa. Meli zitasafirisha bidhaa hizi kutoka Bandari ya Haifa hadi bandari za Ugiriki, Poland, Italia, na Ulaya, na hivyo kuanzisha uhusiano kati ya Ulaya na Asia kwa njia hii.
Baada ya zaidi ya miaka 70 ya juhudi na Marekani na utawala wa Kizayuni, ni nchi chache tu zimeanzisha uhusiano na utawala huo wakati vita vingi na mipango kama Mpango wa Karne, Makubaliano ya Abrahamu, na Mashariki ya Kati Kubwa hazijafanikiwa kuanzisha uhusiano kama huo.
Watafiti katika Jukwaa la Kimkakati la Vyombo vya Habari na Mitandao ya Kijamii walichunguza hotuba ya kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Seyed Ali Khamenei ya Ijumaa, ambapo alitaja mradi wa IMEC, alibainisha.
"Walichunguza jinsi vyombo vya habari katika nchi mbalimbali vilivyojadili maoni ya umma kuhusu uhusiano na Israel, ni diskuru gani walizochukua, na mada gani walizozingatia ili kudumisha idhini ya umma ya kushiriki kwa nchi zao katika mradi huu wa IMEC."
Hosseini Dana alisema watafiti wamefuatilia na kuchambua jinsi vyombo vya habari katika nchi mbalimbali vimewasiliana na watu wa eneo hilo kuhusu ushirikiano wa nchi hizo na Israel na kilichoongoza kwa ushirikiano huo.
"Baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya utawala wa Kizayuni na Hamas huko Gaza kusainiwa, hatua ya kwanza ya utawala huo ilikuwa ni kutuma mwakilishi wake katika UAE kufuatilia njia ya IMEC."
Aliwataka watafiti waliokuwepo kwenye kongamano kushiriki matokeo ya tafiti zao.
Katika hotuba yake, Mohammad Kazem Karami alijadili msimamo wa Uturuki na nafasi ya vyombo vya habari vyake kuhusu njia ya IMEC. Alisema kuwa vyombo vya habari vya Uturuki vimechukua msimamo maalum na ulioratibiwa kuhusu IMEC ikilinganishwa na nchi nyingine.
"IMEC ilipopuuza Uturuki, hisia za nchi hiyo kuhusu njia hiyo ziliongezeka," alisema.
Njia ya IMEC ilitangazwa katika mkutano wa G20, na sababu kuu ya G20 kuzingatia suala hili ilikuwa kuhakikisha usalama wa Israel katika eneo hilo, alisema. "Tunaweza hata kuona kwamba licha ya Operesheni ya Dhoruba ya Al-Aqsa, nchi haziko tayari kuachana nayo na zimezidi kuwa na ujasiri kuhusu hilo."
Aliongeza kuwa njia ya IMEC, zaidi ya kubadilishana kibiashara, inalenga kuhakikisha usalama wa Israel katika eneo hilo. "Mikakati kama Makubaliano ya Abrahamu na miradi mingine ya kawaida ya kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni pia inafuata lengo hili."
Ahmad Hajir Mashouf, mtafiti mwingine katika mkutano huo, alishiriki matokeo yake kutoka kwa kufuatilia vyombo vya habari vya Ugiriki.
Alisema kuwa vyombo vya habari vya Ugiriki vimeanzisha mradi huo kama mpango wa kitaifa, na kufanya faida zake zote kuonekana kwa umma.