IQNA

16:28 - August 16, 2026
Habari ID: 3482630

Waislamu nchini Uingereza wahimizwa kusali Swala ya Istisqa (Swala ya kuomba mvua)

IQNA – Katikati ya ukame usio wa kawaida na uhaba mkali wa maji unaotishia sekta ya kilimo na mazingira, wanazuoni wa Kiislamu nchini Uingereza wametoa wito kwa maimamu wa misikiti na waumini kufufua sunna tukufu ya “Istisqa” (Swala ya kuomba mvua).

Swala ya mvua.

Kwa mujibu wa taarifa, Uingereza inapitia kipindi cha kiangazi kikali, ambapo mamlaka zimebainisha kuwa takriban asilimia 71.3 ya ardhi ya nchi hiyo imeathiriwa na ukame, na mamilioni ya wakazi wanaishi katika maeneo yanayokabiliwa na vikwazo vya matumizi ya maji.

Ripoti zinaonyesha kuwa Uingereza imeshuhudia mwezi wa Julai uliokuwa na ukame mkubwa zaidi katika kipindi cha karibu miaka 190, kutokana na rekodi ya chini ya mvua na kupanda kwa joto kwa kasi, hali ambayo imesababisha kushuka kwa viwango vya maji katika mito na mabwawa, na kusababisha kuwekwa kwa masharti ya matumizi ya maji.

Katika kukabiliana na janga hili, wanazuoni wa Kiislamu wametoa wito kwa maimamu wa misikiti kuongoza Swala ya kuomba mvua kote nchini Uingereza kuanzia tarehe 15 Agosti, ikiwemo kujumuisha dua za mvua katika khutba za Ijumaa na kuswali swala hizo katika viwanja vya wazi.

Wataalamu wanasisitiza kuwa kukabiliana na ukame hakupaswi kuishia katika nyanja ya kiroho pekee, bali pia kunahitaji kuepuka matumizi mabaya ya maji na kulinda rasilimali za asili, sambamba na wito wa serikali wa kuweka akiba na kutumia maji kwa busara.

Wanaongeza kuwa janga hili, pamoja na dhima ya vitendo na ulinzi wa mazingira kwa wajibu, linahitaji unyenyekevu mbele ya Mwenyezi Mungu, kwa matumaini kuwa mvua zitanyesha na rasilimali za maji na kilimo zitahifadhiwa kwa ajili ya vizazi vijavyo.

3498668

Habari zinazohusiana
captcha