IQNA

Mahujaji milioni 2.5 waanza kutekeleza ibada ya hija

16:24 - November 15, 2010
Habari ID: 2032703
Mahujaji milioni mbili na nusu wa nyumba tukufu ya Mwenyezi Mungu wako Arafa kwa ajili ya kutekeleza moja ya nguzo muhimu kabisa katika ibada tukufu ya Hija.
Kisimamo cha Arafa kinahesabiwa kuwa moja ya nguzo muhimu kabisa za ibada ya Hija na kama ilivyonukuliwa katika riwaya ni kwamba, atakayepitwa na kisimamo cha siku ya tarehe 9 Dhil Hijja katika uwanja wa Arafa basi atakuwa hana Hija.
Mahujaji wanatarajiwa kukipitisha kipindi chote cha mchana wakiwa katika uwanja huo wa Arafa wakiomba dua na baada ya kuzama jua wataelekea Muzdalifa.
Aidha leo mahujaji kutoka nchi mbalimbali wameungana na mahujaji wa Kiirani kwa ajili ya kutekeleza marasimu ya kujibari na kujiweka mbali na washirikina katika jangwa la Arafa sambamba na kusomwa ujumbe wa hija ya mwaka huu wa Ayatullah Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu. 695903

captcha