Maandamano hayo ambayo yaliandaliwa na ‘Kampeni ya Mshikamano wa Palestina na Scotland’ ilifanyika pia kulaani jinai za hivi karibuni za utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza na uporaji wa ardhi zaidi za Palestina unaofanywa na utawala huo ghasibu.
Waandamanaji wanasema wameaibishwa na kitendo cha Shirikisho la Soka Scotland kualika timu hiyo ya Israel. Mapmea wachezaji soka Wapalestina walikuwa wametoa wito wa kususiwa mechi hiyo kutokana na ugaidi unaotendwa na utawala haramu wa Israel dhidi ya wanamichezo Wapalestina.