IQNA

Nchi 75 kushiriki mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu nchini Iran

18:25 - May 09, 2016
Habari ID: 3470302
Nchi 74 zitatuma wawakilishi katika Mashidano ya Kimataifa ya Qur'ani ambayo yanaanza wik hii, Tehran mji mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Hayo yamedokezwa na Hujjatul Islam wal Muslimin Ali Mohammadi Mwakilishi wa Faqihi Mtawala na Mkuu wa Shirika la Awqaf la Iran. Akizungumza na waandishi habari Jumatatu mjini Tehran, amesema kutakuwa na washiriki 130 kutoka nchi 75 katika Mashindano ya 33 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran.
Amesema kwa mara ya kwanza mashindano yatafanyika katika Ukumbi Mkubwa wa Sala wa Imam Khomeini MA, ili kuwezesha idadi kubwa ya wananchi kujumuika katika mashindano hayo.

Sheikh Mohammadi ameongeza kuwa, mashindano ya mwaka huu yatakuwa na washiriki kutoka mabara ya Afrika, Asia, Ulaya, Marekani na Oceania.

Ameongeza kuwa mashindano hayo yatakuwa na washiriki 57 katika kategoria ya kuhifadhi Qur'ani kikamilifu na wengine 57 katika kategoria ya qiraa. Aidha amesema mwaka huu kutakuwa kitengo maalumu cha washiriki 16 wenye ulemavu wa macho.

Sheikh Mohammadi amebaini kuwa mashindano ya mwaka huu yatakuwa na majaji 10 wa kigeni na 8 kutoka Iran.


Aidha amesema washiriki wa mashindano hayo watapata pia fursa ya kukutana na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu.

Mashindano ya 33 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran yataanza Jumatano wiki hii kuanzaia tarehe 11 hadi 17 Mei.
Rais Hassan Rouhani wa Iran anatazamiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mashindano ya mwaka huu.
3496012
Kishikizo: mashindano
captcha