Ezzedine Mihoubi amesema kuwa kanali hiyo ya televisheni itaanza kutangaza kwa masaa manane kwa siku na kwamba wakati huo utaongezwa kadiri muda unavyopita.
Amesema kuwa miongoni mwa ratiba za televisheni hiyo ni kutoa mafunzo ya kuhifadhi na kusoma Qur'ani Tukufu, hotuba za maulamaa wa Kiislamu kuhusu matatizo ya jamii ya Kiislamu na vipindi vya kiutamaduni. Lugha ya Tamazight ni mojawapo ya lugha za Mabarbari wanaoishi katika nchi za kaskazini mwa Afrika. 372328