Maulana alizaliwa katika mji wa Balkh na akiwa bado mtoto alienda katika mji wa Samarqand lakini baada ya muda mfupi aliondoka katika mji huo na kuelekea katika mji wa Konya nchini Uturuki.
Mashairi ya Maulana ni mashuhuri kwa kumsifu Mwenyezi Mungu na kutumia mifano ya Qur'ani Tukufu. Kitabu chake cha Masnavi, au Masnavi-ye-Ma'navi ni athari yake iliyovuma sana.
Maulana aliugua homa kali na kuaga dunia mwaka 1273 Miladia akiwa na umri wa miaka 59 na alizikwa katika mji wa Konya.