IQNA

Mwili wa qarii wa Qur'ani Misri wabakia salama miaka mitano baada ya kifo chake + Video

TEHRAN (IQNA)- Qarii maarufu wa Misri Abdul Fattah Tartouti amesimulia kisa cha ajabu cha qarii mwenzake marhum Muhammad al-Laythi.

"Sheikh Muhammad al Laythi alifariki miaka mitano mapema kabla ya baba yake. Wakati baba yake alipofariki, kaburi alimokuwa Laythi lilifunguliwa ili baba yake azikwe," anasimulia Sheikh Tarouti.

Anaendelea kusema kuwa: "Mhusika katika masuala ya makaburi akiwa mle ndani akiwa na hali ya mshangano alimuita mmoja ya marafikizi Laythi na kumuambia, 'njoo umtizame rafiki yako."

Walitizama vidole vyake  vilkuwa vimenyooka  na mikono ilikuwa haina mabadiliko yoyote na mwili wake pia walipougusa walihisi hauna mabadiliko yoyote na umebakia salama."  

Sheikh Muhammad Muhammad al-Laythi alizaliwa mwaka 1949 katika familia ya wasomaji na wanaohifadhi Qur'ani katika  mkoa wa Ash Sharqia ambapo alijifunza Qur'ani akiwa yungali mtoto.

Alijifunza qiraa ya Qur;ani kutoka kwa baba yake na maustadhi wengine katika mkoa huo na kisha akajiunga na Radio ya Qur'ani ya Misri kama qarii mwaka 1984. Aliwahi kushiriki katika vikao vya kusoma Qur'ani katika nchi nyingi duniani kama vile Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, India, Pakistan, Ujerumani na Afrika Kusini. Aliaga dunia Machi 5 2006.

4021782

Kishikizo: al laythi ، qurani tukufu ، tarouti