qurani tukufu

IQNA

IQNA – Zaidi ya watu 10,000 wametembelea Kituo cha Uchapishaji wa Qur’an Tukufu cha Mfalme Fahd kilichopo Madina wiki iliyopita.
Habari ID: 3482636   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/17

IQNA – Msomaji mashuhuri wa Qur’an Tukufu kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ndugu Masoud Panjeh, ambaye ni Qari katika Haram Tukufu ya Imam Ali ibn Musa al-Ridha (AS) mjini Mashhad, hivi karibuni amesoma aya za 1–8 za Surah Al-Mulk.
Habari ID: 3482635   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/17

IQNA – Mwanazuoni wa Kiislamu kutoka Iran ametoa wito wa kuitumia Akili Mnemba (Artificial Intelligence - AI) siyo kama nyenzo ya kusaidia pekee, bali kama chachu kuu ya kuleta mageuzi katika tafiti na harakati za Qur’ani.
Habari ID: 3482634   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/16

IQNA – Kambi inayojumuisha mashindano matatu ya usomaji wa Qur’ani (Tilawa), warsha za ufundishaji, na hafla maalum ya watoto imepangwa kufanyika huko Mahibadhoo, mji wa kisiwani ulioko katikati mwa nchi ya Maldives.
Habari ID: 3482631   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/16

IQNA – Wananchi katika mkoa wa Marib nchini Yemen wamefanya maandamano na matukio ya kulaani vitendo vya kuvunjiwa heshima Qur’ani katika nchi za Magharibi.
Habari ID: 3482629   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/15

IQNA – Shule ya Qur’ani ya ‘Gaza’ iliyoko katika mkoa wa Hama Bouziane, jimbo la Constantine nchini Algeria, imejitolea kwa miaka 24 kufundisha na kuwezesha kuhifadhi Qur’ani Tukufu. Taasisi hii imekuwa mwanga wa maarifa na malezi ya kiroho, ikitoa mafunzo kwa mamia ya wahifadhi wa kiume na wa kike.
Habari ID: 3482627   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/15

IQNA – Akilaani vitendo vya mara kwa mara vya kuidhalilisha na kuivunjia heshima Qur’ani Tukufu kama vitendo vya “Kizayuni na Kimarekani,” kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen, Sayyid Abdul-Malik Badruddin al-Houthi, amesema vitendo hivyo vya kukufuru na kukiuka heshima ya Qur’ani ni sehemu ya uadui mpana zaidi dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3482622   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/14

IQNA – Mafunzo ya majira ya joto ya Qur’ani Tukufu kwa wasichana yameanza katika Haram Tukufu ya Imam Hussein (AS) mjini Karbala, Iraq.
Habari ID: 3482621   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/14

IQNA – Siku ya pili ya mashindano ya Qur'ani Tukufu ya Dawlet El Telawa nchini Misri ilishuhudia uwezo mkubwa na maonyesho ya kuvutia kutoka kwa washiriki kadhaa.
Habari ID: 3482616   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/12

IQNA – Kundi la wanawake vijana wa Kiislamu katika Kitivo cha Tiba cha Chuo Kikuu cha Sarajevo limekuwa ishara ya muunganiko kati ya utambulisho wa kidini na ubora wa kielimu. Wamepata heshima kuu za kielimu pamoja na mafanikio bora katika kuhifadhi Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 3482614   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/11

Inna Lillah wa Inna Ilayhi Rajioun
IQNA – Rais wa Umoja wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu (IUMS) ametoa rambirambi zake kwa watu wa Algeria na Ummah ya Kiislamu kufuatia kuaga dunia kwa mwanazuoni mkuu wa Qur’ani, Sheikh Mohamed Said Kaabash.
Habari ID: 3482611   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/10

IQNA – Yousef, kijana kutoka Bahira nchini Misri, amewavutia wengi kwa sauti yake ya usomaji Qur’ani Tukufu na ameendeleza kipawa chake kwa kusikiliza qiraa za maqari mashuhuri kupitia mtandao. Anaota ndoto siku moja kuwa miongoni mwa majina makubwa katika uwanja wa usomaji wa Qur’ani na kufuata nyayo za Sheikh Abdul Basit Abdul Samad.
Habari ID: 3482609   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/10

IQNA – Katika kile kinachothibitisha kuwa nuru ya Qur’ani Tukufu haina mipaka, Mahmoud Hassan Ashrafi, kijana mwenye umri wa miaka 18 kutoka Bangladesh ambaye ana ulemavu wa macho na hivyo haoni, anashiriki katika hatua ya fainali ya Mashindano ya 46 ya kimataifa ya Qur’ani Tukufu huko Makka, Saudia.
Habari ID: 3482608   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/10

IQNA – Toleo la tatu la programu ya “Nyoyo Zilizoshikamana na Misikiti” (Hearts Attached to Mosques) limepangwa kuzinduliwa huko Sharjah katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
Habari ID: 3482607   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/10

IQNA – Kupokea vijana Waislamu na kuwapatia programu za kidini na Qur’ani huifanya misikiti nchini Brazil kuimarisha hali yao ya kiroho, huku pia ikilea kizazi kipya kilichounganishwa na Qur’an na Sunna ya Mtume SAW.
Habari ID: 3482606   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/09

IQNA – Kumbi za mashindano jijini Makka zilisikika zikirindima kwa sauti za kuvutia za usomaji wa aya tukufu za Qur’an siku ya Jumamosi, huku washiriki 33 wa kwanza wakijitokeza mbele ya jopo la majaji.
Habari ID: 3482602   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/09

IQNA-Katika mwendelezo wa kuonyesha ustahimilivu na ari ya kiimani katikati ya mapambano, wanafunzi 110 wa kike wenye kuhifadhi Qur’ani huko Gaza wamefanikiwa kuhitimisha usomaji wa Qur’ani nzima katika kikao kimoja cha Khatm al-Qur’an.
Habari ID: 3482585   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/04

IQNA – Waziri wa Awqaf wa Misri ametoa ujumbe wa rambirambi kufuatia kifo cha Sheikh Saeed al-Najjar, msomaji mkongwe zaidi wa Qur’ani katika Mkoa wa Gharbia.
Habari ID: 3482584   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/04

IQNA – Taasisi ya Kijiji cha Utamaduni (Katara) nchini Qatar imefungua milango ya maombi kwa ajili ya Toleo la 10 la Tuzo ya Usomaji wa Qur’ani Tukufu. Mashindano hayo ya Qur’ani yanafanyika chini ya kauli mbiu: “Kuimarisha Sauti za Usomaji Mwema”.
Habari ID: 3482583   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/04

IQNA – Akisisitiza mwitikio mzuri wa programu za Qur'ani Tukufu miongoni mwa mazuwaru wakati wa matembezi ya Arbaeen, msomaji mashuhuri wa Qur'ani kutoka Iran ametoa wito wa kuongezwa kwa idadi ya programu hizo.
Habari ID: 3482581   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/03