qurani tukufu

IQNA

IQNA-Katika kasri maarufu la Topkapi jijini Istanbul, utamaduni wa kale wa Kiislamu wa usomaji wa Qur'ani Tukufu umeendelea bila kukoma kwa karne nyingi. Usomaji huu wa kila siku, ulioanzishwa na Masultani wa Uthmaniyya, unaendelea hadi leo kama sehemu ya urithi wa kiroho na kitamaduni wa Waislamu wa eneo hilo.
Habari ID: 3481477    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/06

IQNA-Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar nchini Misri kimezindua awamu ya kwanza ya mashindano ya kila mwaka ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu, maarufu kama Mashindano ya Sheikh Al-Azhar. Zaidi ya washiriki 150,000 wa kiume na wa kike kutoka mikoa mbalimbali ya Misri wanashiriki katika awamu hii ya mwanzo.
Habari ID: 3481476    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/06

IQNA – Shorouk Marar ni mwanamke kutoka mji wa Beit Daqo, kaskazini-magharibi mwa al-Quds (Jerusalem) inayokaliwa kwa mabavu, ambaye ana kisa cha azma thabiti na imani ya kina.
Habari ID: 3481475    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/05

IQNA – Chuo Kikuu cha Houston kilichopo jimbo la Texas, Marekani, kimetangaza kuwa kinachunguza tukio la kuvunjia heshima nakala ya Qur'an Tukufu wakati wa mkusanyiko wa wanafunzi Waislamu.
Habari ID: 3481472    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/05

Ushirikiano Katika Qur'ani/ 8
IQNA-Katika Uislamu, kuna kanuni inayoitwa ta’āwun , yaani kushirikiana katika mambo ya kheri. Waislamu wanapaswa kusaidiana katika mema, lakini wajiepushe kushirikiana katika dhulma, uonevu, au mambo ya batili; hata kama anayehusika ni ndugu au rafiki wa karibu.
Habari ID: 3481467    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/04

IQNA – Sherehe maalum ya kuwatunuku wahifadhi wa Qur’ani Tukufu kutoka Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar imefanyika katika mkoa wa Giza nchini Misri.
Habari ID: 3481464    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/04

IQNA – Waziri wa Awqaf wa Algeria, Youssef Belmahdi, ametangaza kukamilika kwa kozi ya tatu ya mafunzo kwa majaji wa mashindano ya Qur’ani Tukufu nchini humo.
Habari ID: 3481457    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/03

IQNA – Chuo Kikuu cha Gujrat, Kampasi ya Hafiz Hayat, nchini Pakistan kimeandaa semina maalum yenye kichwa cha habari “Dhana ya Muda kwa Mujibu wa Qur’ani Tukufu,” ikiwaleta pamoja wanafunzi kwa ajili ya maarifa ya kiakili na kiroho.
Habari ID: 3481453    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/02

IQNA – Lengo la elimu ya Qur’ani linapaswa kwenda mbali zaidi ya kuhifadhi, kuelekea kuunda “watu wa mfano wa Qur’ani hai” wanaoathiri jamii kupitia mwenendo wao, asema Hujjatul-Islam Seyyed Mohammad-Mehdi Tabatabaei kutoka Iran.
Habari ID: 3481450    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/02

Ushirikiano katika Qur’ani Tukufu/7
IQNA – Msingi wa jamii ni ushirikiano, kushirikiana, na kubadilishana manufaa. Kwa hivyo, mtazamo wa kielimu wa Kiislamu umechukulia ushirikiano kuwa miongoni mwa mahitaji ya fikra za kimaadili.
Habari ID: 3481448    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/01

IQNA – Kituo cha Maendeleo ya Elimu kwa Wanafunzi wa Kigeni katika Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Al-Azhar nchini Misri kimetangaza uzinduzi wa matawi mawili mapya ya Shule ya Kuhifadhi na Kusoma Qur’ani ya Imam el-Tayeb.
Habari ID: 3481445    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/01

IQNA – Akifafanua dhana ya Yawm At-Taghābun, mwanazuoni wa chuo kikuu cha kidini kutoka (Hawzah) Iran amesema kuwa katika Siku ya Kiyama, mtu ataonyeshwa si tu matokeo ya matendo yake, bali pia mahali pake palipopotea Peponi—mandhari itakayokuwa majuto makubwa na mateso ya kiroho yasiyoelezeka.
Habari ID: 3481443    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/01

IQNA – Mhubiri wa Kiislamu mzaliwa wa Japani, Fatima Atsuko Hoshino, amesema kuwa Qur'ani Tukufu imempa majibu ya maswali aliyokuwa nayo kwa muda mrefu na imemponya maradhi ambayo wataalamu wa tiba walishindwa kuyatibu.
Habari ID: 3481442    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/31

IQNA – Serikali ya Malaysia imezindua mfumo mpya uitwao iTAQ unaotumia teknolojia ya Akili Mnemba (AI) kuharakisha mchakato wa kuthibitisha usahihi wa machapisho ya nakala za Qur'ani Tukufu.
Habari ID: 3481441    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/31

IQNA – Mwanazuoni wa masuala ya dini, Reza Malazadeh Yamchi, amesema kuwa Qur'ani Tukufu inatoa msingi wa maadili kwa uelewano baina ya tamaduni, ikisisitiza heshima, usawa, na mazungumzo badala ya ubabe wa kitamaduni.
Habari ID: 3481440    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/31

IQNA – Mwenyekiti wa Umoja wa Wanachuoni wa Qur'ani wa mkoa wa Kafr el-Sheikh nchini Misri amempa heshima maalum Sheikh Mohammed Younis al-Ghalban, gwiji wa usomaji wa Qur'an.
Habari ID: 3481439    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/31

IQNA – Mashindano ya Tatu ya Kitaifa ya Qur'an nchini Kyrgyzstan yametamatika rasmi kwa hafla maalum iliyofanyika siku ya Jumatano.
Habari ID: 3481438    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/31

IQNA – Mashindano makubwa ya Qurani yatakayoshirikisha washiriki kutoka ndani na nje ya nchi huko Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) yataanza rasmi tarehe 1 Novemba.
Habari ID: 3481437    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/29

IQNA – Mafanikio ya kihistoria katika sanaa ya hati za Kiislamu yamezinduliwa mjini Istanbul: Ni nakala kubwa zaidi ya Qur'ani duniani iliyoandikwa kwa mkono, matokeo ya juhudi za miaka sita bila kukata tamaa.
Habari ID: 3481436    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/29

IQNA – Jumuiya ya Qur'ani Tukufu ya Mauritania imetangaza uzinduzi wa kampeni ya kusambaza nakala 50,000 za Qurani nchini humo.
Habari ID: 3481434    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/29