qurani tukufu

IQNA

IQNA – Mwanamke kutoka mji wa Qena, Misri, ameweza kuhifadhi Qur’an Tukufu kikamilifu akiwa na umri wa miaka 80, licha ya kutokuwa na elimu ya kusoma na kuandika.
Habari ID: 3481541    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/19

IQNA – Sharjah imezindua Tamasha la 26 la Sanaa za Kiislamu, tukio la siku 70 linaloangazia urithi wa sanaa za Kiislamu kutoka duniani kote.
Habari ID: 3481540    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/19

IQNA – Waandamanaji waligongana mitaani Dearborn Jumanne baada ya wanaharakati wa mrengo wa kulia kuwachokoza wakazi kwa kauli za chuki dhidi ya Uislamu na wahamiaji, na kujaribu kudhalilisha Qur'ani Tukufu. Tukio hilo lilisababisha msuguano mdogo na polisi kuingilia kati kwa nguvu ili kuwatenganisha makundi hayo.
Habari ID: 3481539    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/19

IQNA – Warsha ya mafunzo kuhusu mbinu na njia za kuhifadhi na kukarabati nyaraka za kale za Qur'ani Tukufu za mwanzo imefanyika nchini Yemen.
Habari ID: 3481538    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/19

IQNA – Idara ya Awqaf (Wakfu) katika Mkoa wa Tafilah, Jordan, imeanzisha mradi maalumu wa kukusanya na kurekebisha nakala za Qur'ani Tukufu zilizochakaa na kuharibika kutoka misikiti ya nchi hiyo.
Habari ID: 3481537    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/19

Ushirikiano Katika Qur’ani Tukufu / 12
IQNA – Mojawapo ya matumizi muhimu ya kanuni ya ushirikiano ni katika uwanja wa uchumi, ingawa uhusiano kati ya kanuni ya ushirikiano katika Qur’ani na uchumi wa ushirika uko zaidi katika kiwango cha kufanana kwa maneno. Qur’ani inatoa msingi unaoweza kutumika katika nyanja mbalimbali, ikiwemo uchumi.
Habari ID: 3481535    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/18

IQNA – Kipindi cha kwanza cha televisheni Dawlat al-Tilawa kilizinduliwa Ijumaa nchini Misri, kikiwa safari mpya ya kugundua vipaji vinavyochipukia katika kisomo cha Qur’ani na Tajweed.
Habari ID: 3481534    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/18

IQNA – Mwanafalsafa kutoka Algeria amesema jamii za Kiislamu zinakabiliwa na mgogoro wa kimaadili unaotishia familia na kupotosha ufahamu wa Kiislamu kuhusu wanawake, maadili na uhalisia wa kisasa.
Habari ID: 3481533    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/18

IQNA – Qari wa kimataifa kutoka Iran amesema kuwa kisomo cha mashindano mengi kina upungufu wa kina cha hisia, na ametoa rai ya kuwepo kwa viwango vya wazi vitakavyosaidia kuelekeza ubunifu katika kisomo cha Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 3481532    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/18

IQNA – Maqari wa kike wa Qur’ani kutoka Dar-ul-Qur’an ya Astan ya Haram Tukufu ya Imam Hussein (AS) wameibuka washindi katika mashindano ya saba ya kitaifa ya wanawake wa Qur’ani nchini Iraq.
Habari ID: 3481531    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/17

IQNA-Duru ya tatu kwa mashindano ya kila mwaka ya Qur’ani nchini Nepal imeingia hatua ya mwisho, Jumapili. Wizara ya Mambo ya Kiislamu, Da‘wa na Mwongozo ya Saudi Arabia imezindua raundi ya mwisho ya mashindano ya kuhifadhi Qur’ani kwa wavulana na wasichana katika mji mkuu wa Katmandu, ulioko Asia Kusini.
Habari ID: 3481530    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/17

IQNA – Kipindi cha televisheni Dawlet El Telawa, mashindano maalum ya vipaji vya usomaji wa Qur’ani nchini Misri, kimemkumbuka Qari maarufu Sheikh Mahmud Khalil al‑Hussary.
Habari ID: 3481526    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/16

IQNA – Je, ni vipi maandishi ya kidini kama Qur’ani Tukufu  yanaweza kuthibitishwa kuwa sahihi na kusomwa kwa kutumia akili mnemba (AI) ya kisasa?
Habari ID: 3481525    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/16

IQNA-Vehbi Ismail Haki (1919–2008) alikuwa mwandishi, imam na msomi mashuhuri kutoka Albania aliyechangia pakubwa kusambaza utamaduni wa Kiislamu na maarifa ya Qur’ani kwa watu wa taifa lake kupitia maandiko kwa Kiarabu, Kiingereza na Kialbania. Alizaliwa Shkodra, mji wa kaskazini wenye historia ndefu ya elimu ya Kiislamu tangu enzi za Waothmani.
Habari ID: 3481523    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/16

Ushirikiano katika Qur’ani Tukufu / 11
IQNA – Ushirikiano na watu binafsi pamoja na taasisi zinazojitahidi kuandaa mazingira ya ndoa na kuundwa kwa familia kwa vijana ni miongoni mwa mifano dhahiri ya ushirikiano wa kijamii.
Habari ID: 3481521    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/15

IQNA – Katika ujumbe wake kwa washiriki wa mashindano ya 17 ya kitaifa ya Qur’ani “Mudha Mattan”, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, ameyataja mashindano hayo kuwa ni uwanja wa kukuza ushirikiano, huruma, na kuendeleza stadi mbalimbali za kufanya kazi kwa pamoja.
Habari ID: 3481519    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/15

Qur’ani ni Chemchemi ya Maarifa
IQNA – Mwanazuoni maarufu wa Kiislamu nchini Iran amesisitiza kuwa akili mnemba (AI) inapaswa kutumika kwa lengo la kuendeleza Qur’ani Tukufu, akibainisha kuwa jukumu hilo ni huduma muhimu ya kielimu kwa Uislamu.
Habari ID: 3481517    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/15

IQNA – Wavamizi wa Kizayuni wasiokuwa halali waliharibu msikiti katika mji wa Deir Istiya, Ukingo wa Magharibi, usiku wa Alhamisi, wakichoma sehemu za ndani na kuharibu nakala kadhaa za Qur’ani Tukufu katika shambulio la dharau lililoambatana na maandiko ya vitisho.
Habari ID: 3481516    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/14

IQNA – Qur’an Tukufu ni ramani ya kuishi maisha mema, amesema mwanazuoni wa Kiislamu nchini Iran, akiongeza kuwa wale wanaoshikamana zaidi na Qur’ani huishi maisha ya heri na ya uadilifu yanayopendeza kwa Mwenyezi Mungu.
Habari ID: 3481515    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/14

IQNA – Wizara ya Awqaf na Mambo ya Kiislamu ya Qatar imezindua maonyesho ya Qur’an sambamba na toleo la 30 la Mashindano ya Qur’an ya Sheikh Jassim bin Mohammed Al Thani mjini Doha.
Habari ID: 3481514    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/14