IQNA

Idi za Mwezi wa Shaaban katika Haram ya Imam Hussein AS mjini Karbala

TEHRAN (IQNA)- Haram Takatfu ya Imam Hussein AS mjini Karbala Iraq ni mwenyeji wa maelefu ya wafanya ziyara katika wakati huu wa Idi za Mwezi wa Shaaban.
Kila mwaka sherehe huandaliwa katika maeneo mbali mbali ya dunia kwa mnasaba wa kukumbuka kuzaliwa Imam Hussein AS, Hadhrat Abbas AS na Imam Sajjad AS ambazo huangukia katika siku za tatu, nne na tano za Mwezi wa Shaaban.