IQNA

Hali baada ya mitetemeko ya ardhi Uturuki na Syria

TEHRAN (IQNA)- Uturuki na Syria jana zimekumbwa na mitetemeko miwili mikubwa ya ardhi. Mtetemeko wa kwanza ulikuwa na ukubwa wa 7.8 kwa kipimo cha rishta na umetokea saa kumi na dakika 17 alfajiri ya leo kwa saa za eneo hilo.

Kitovu chake kilikuwa ni katika mji wa Gaziantep wa Uturuki ambapo mamia ya majengo yameporomoka.Masaa machache baadaye kulijiri mtetemeko mwingine wa ardhi uliokuwa na ukubwa 7.6 kwenye kipimo cha rishta. Picha hizi zinaonyesha hali baada ya mitetemeko hiyo ambayo imepelekea maelfu ya watu kupoteza maisha na uharibifu mkubwa.