Tamaduni hiyo ilifanywa kwa joto kali la kiangazi na inaweza kuvunja rekodi kulingana na idadi ya mahujaji.
Jua lilipochomoza, makundi ya waabudu walikariri aya kutoka kwenye Qur'an Tukufu kwenye mwinuko wa mawe, ambapo Mtume Mohammad (s.a.w.w) alitoa khutba yake ya mwisho.
Hija hii ya kila mwaka inachukuliwa kuwa ibada muhimu zaidi, na baada ya miaka mitatu ya vizuizi vya Covid 19 maafisa wanatarajia kuwa kubwa zaidi kwenye rekodi.
Hija huvutia zaidi ya mahujaji milioni 2.5, na kuifanya kuwa moja ya mikusanyiko ya kidini iliyoenea zaidi ulimwenguni.
Joto lilipanda hadi nyuzi joto 46 siku ya Jumatatu, na wafanya Ibada waliovalia kanzu walikusanyika chini ya miavuli walipokuwa wakisafiri kutoka Makka hadi Mina, ambako walilala katika jiji kubwa lenye mahema kabla ya ibada katika Mlima Arafat.