Kwa mujibu wa taarifa, Wapalestina waliokuwa na hasira pamoja na viongozi kadhaa wa makundi ya Kipalestina siku ya Jumatatu walishiriki katika maandamano makubwa katika maeneo kama vile Al Khalil, Tulkaram na Tubasi na kubainisha upinzani wao kwa mpango wa utawala wa Kizayuni wa kukalia kwa mabavu eneo la Ukingo wa Magharibi. Maandamano hayo yamefanyika kwa mnasaba wa mwak wa 53 wa Naksa au siku ambayo Wapalestina walipata pigo. Washiriki walitoa nara kama vile 'Tunapinga kupora ardhi' , 'Ardhi ni ya taifa letu, na 'Tutakufa ili Palestina iwe Hai'.