IQNA

Wapalestina Ghaza walaani hatua ya Israel kufunga eneo la Al-Aqsa

TEHRAN (IQNA) - Mamia ya Wapalestina wameandamana katika Ukanda wa Ghaza kulaani hatua ya mahakama ya utawala haramu wa Israel kufunga lango la Bab al-Rahma la Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem).

Waandamanaji walikuwa wamebeba mabango yaliyokuwa na maandishi kama vile " Tutalinda Quds Kwa Damu Zetu", "Mshikamano na Watu wa Quds', na 'Tunaunga Mkono Bab al Rahma"

 
 
Kishikizo: ghaza ، palestina