IQNA – Mahmoud Khalil, mwanaharakati M palestina , amekata rufaa katika Mahakama Kuu ya Marekani ili kuzuia kufukuzwa kwake nchini humo.
Habari ID: 3482279 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/24
IQNA – Kuanzia Gaza hadi Catalonia, Pep Guardiola amedhihirisha kuwa anaamini mambo makubwa zaidi ya soka. Kocha huyo wa Manchester City amejipatia sifa duniani kama mmoja wa watu mashuhuri wanaosimama kidete kutetea haki za watu wa Palestina.
Habari ID: 3482274 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/23
IQNA – Watetezi wa haki za binadamu na maafisa wa Palestina wameilaani hatua wanayoieleza kuwa ni kukiuka kwa mfumo uhuru wa ibada, baada ya utawala haramu wa Israel kwa mara nyingine kuzuia maelfu ya Wa palestina wa Gaza kusafiri kwenda Saudi Arabia kwa ajili ya Hija ya kila mwaka.
Habari ID: 3482268 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/22
IQNA – Mchezaji wa Ufaransa, Sacha Bouy, alivutia hisia wakati wa sherehe za ubingwa wa Ligi ya Uturuki za klabu yake Galatasaray, alipohudhuria hafla ya kukabidhiwa kombe akiwa amebeba bendera ya Palestina.
Habari ID: 3482254 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/18
IQNA – Mlipuko mkubwa umetokea katika kituo cha viwanda katika eneo la Beit Shemesh karibu na mji mtakatifu wa Al‑Quds (Jerusalem), huku mtikisiko wake ukihisiwa katika maeneo mbalimbali ya ardhi zinazokaliwa kwa mabavu ambazo zimepachikwa jina la 'Israel'.
Habari ID: 3482248 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/17
Maafisa wa UN katika Siku ya Ukumbusho wa Nakba
IQNA – Wakikumbuka mwaka wa Nakba Ijumaa, maafisa wakuu wa Umoja wa Mataifa wameonya kwamba mateso na uhamishaji walioupata Wa palestina tangu mwaka 1948, baada ya ardhi yao kukoliniwa na Israel, ni maumivu yanayoendelea kwa vizazi na maelfu ya kilomita.
Habari ID: 3482243 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/16
IQNA – Uamuzi wa nyota wa soka wa Hispania, Lamine Yamal, kupeperusha bendera ya Palestina wakati wa gwaride la ushindi wa Barcelona katika La Liga umeibua wimbi kubwa la uungwaji mkono duniani.
Habari ID: 3482237 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/13
IQNA – Katika kumbukumbu ya tukio lenye kuhuzunisha, shirika la Amnesty International limeilaani vikali utawala wa Israel kwa kuendelea kumshikilia daktari wa Gaza, Dkt. Hussam Abu Safiya.
Habari ID: 3482229 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/12
IQNA – Msafara wa meli unaojulikana kama Global Sumud Flotilla, unaolenga kuvunja mzingiro uliowekwa na utawala katili wa Israeli dhidi ya Wa palestina katika Ukanda wa Gaza, umefika katika maji ya kimataifa karibu na pwani ya Ugiriki.
Habari ID: 3482179 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29
IQNA – Sheikh Raed Salah na Sheikh Kamal al‑Khatib wamelaani marufuku ya wiki moja iliyowekwa na mamlaka za utawala haramu wa Israel kuwazuia kuingia katika Msikiti wa Al‑Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala huo, wakisema ni “shambulio dhidi ya dini yetu.”
Habari ID: 3482178 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29
IQNA – Wakielezea kama uhamasishaji mkubwa zaidi wa aina yake, wanaharakati wa kimataifa wametangaza mipango ya kupeleka meli 200 katika msafara wa misaada unaojulikana kama Freedom and Sumud Flotilla, wakilenga Ukanda wa Gaza katika majira ya kuchipua mwaka huu.
Habari ID: 3482002 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/27
IQNA — Wizara ya Awqaf na Masuala ya Kiislamu ya Palestina imetangaza mpango jumuishi wa kuukaribisha na kuadhimisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika Msikiti wa Al‑Aqsa, uliopo katika mji mtakatifu wa al‑Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na Israel.
Habari ID: 3481954 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/18
IQNA-Kiongozi wa harakati ya Muqawama (mapambano ya Kiislamu) ya Ansarullah nchini Yemen amesema kuwa Marekani na Utawala wa Israel zinakabiliana na Iran kwa sababu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasimama kama kizuizi dhidi ya mradi wao mpana wa kutawala eneo la Asia Magharibi au Mashariki ya Kati.
Habari ID: 3481932 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/14
IQNA – Ziara rasmi ya rais wa utawala wa Israel, Isaac Herzog, nchini Australia ilikumbwa na maandamano makubwa siku ya Jumatatu, huku maelfu ya waandamanaji wakijitokeza katika miji kadhaa, hali iliyopelekea kuwepo makabiliano na polisi.
Habari ID: 3481918 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/11
IQNA – Idadi kubwa ya raia wa Morocco walifanya mkusanyiko mbele ya jengo la Bunge katika mji mkuu Rabat, Ijumaa jioni, wakieleza mshikamano wao na wananchi wa Palestina na kulaani mzingiro unaoendelea kuwekwa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3481901 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/08
IQNA – Katika ishara ya kimaadili na ya kidiplomasia inayoonesha mshikamano na watu wa Palestina, Rais wa Brazil Luiz Inácio Lula da Silva alivaa keffiyeh ya Ki palestina .
Habari ID: 3481899 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/07
IQNA — Mufti Mkuu wa Oman amekosoa vikali ukimya na kutochukua hatua kwa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) pamoja na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) kuhusu uhalifu unaoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wa palestina .
Habari ID: 3481885 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/03
IQNA-Maelfu kwa maelfu ya watu wamejitokeza mitaani katika nchi kadhaa za Ulaya kushiriki maandamano ya kuunga mkono Palestina, huku wakiushutumu utawala dhalimu wa Israel kwa kukiuka mara kwa mara makubaliano ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza kati yake na Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas.
Habari ID: 3481878 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/01
IQNA –Afrika Kusini imemtangaza kaimu balozi wa utawala wa Isarel nchini humo kuwa mtu asiyehitajika na kuamuru afukuzwe mara moja.
Habari ID: 3481876 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/31
IQNA – Pep Guardiola kocha wa timu ya Ligi Kuu ya Soka Uingereza (EPL), Manchester City, ameeleza hadharani uungaji mkono wake kwa wananchi wa Palestina, akielekeza macho ya ulimwengu kwenye janga kubwa la kibinadamu linaloikumba Gaza, wakati wa tukio la hadhara lililofanyika hivi karibuni.
Habari ID: 3481871 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/30