palestina

IQNA

IQNA – Msafara wa meli unaojulikana kama Global Sumud Flotilla, unaolenga kuvunja mzingiro uliowekwa na utawala katili wa Israeli dhidi ya Wa palestina katika Ukanda wa Gaza, umefika katika maji ya kimataifa karibu na pwani ya Ugiriki.
Habari ID: 3482179    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29

IQNA – Sheikh Raed Salah na Sheikh Kamal al‑Khatib wamelaani marufuku ya wiki moja iliyowekwa na mamlaka za utawala haramu wa Israel kuwazuia kuingia katika Msikiti wa Al‑Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala huo, wakisema ni “shambulio dhidi ya dini yetu.”
Habari ID: 3482178    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29

IQNA – Wakielezea kama uhamasishaji mkubwa zaidi wa aina yake, wanaharakati wa kimataifa wametangaza mipango ya kupeleka meli 200 katika msafara wa misaada unaojulikana kama Freedom and Sumud Flotilla, wakilenga Ukanda wa Gaza katika majira ya kuchipua mwaka huu.
Habari ID: 3482002    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/27

IQNA — Wizara ya Awqaf na Masuala ya Kiislamu ya Palestina imetangaza mpango jumuishi wa kuukaribisha na kuadhimisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika Msikiti wa Al‑Aqsa, uliopo katika mji mtakatifu wa al‑Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na Israel.
Habari ID: 3481954    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/18

IQNA-Kiongozi wa harakati ya Muqawama (mapambano ya Kiislamu) ya Ansarullah nchini Yemen amesema kuwa Marekani na Utawala wa Israel zinakabiliana na Iran kwa sababu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasimama kama kizuizi dhidi ya mradi wao mpana wa kutawala eneo la Asia Magharibi au Mashariki ya Kati.
Habari ID: 3481932    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/14

IQNA – Ziara rasmi ya rais wa utawala wa Israel, Isaac Herzog, nchini Australia ilikumbwa na maandamano makubwa siku ya Jumatatu, huku maelfu ya waandamanaji wakijitokeza katika miji kadhaa, hali iliyopelekea kuwepo makabiliano na polisi.
Habari ID: 3481918    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/11

IQNA – Idadi kubwa ya raia wa Morocco walifanya mkusanyiko mbele ya jengo la Bunge katika mji mkuu Rabat, Ijumaa jioni, wakieleza mshikamano wao na wananchi wa Palestina na kulaani mzingiro unaoendelea kuwekwa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3481901    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/08

IQNA – Katika ishara ya kimaadili na ya kidiplomasia inayoonesha mshikamano na watu wa Palestina, Rais wa Brazil Luiz Inácio Lula da Silva alivaa keffiyeh ya Ki palestina .
Habari ID: 3481899    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/07

IQNA — Mufti Mkuu wa Oman amekosoa vikali ukimya na kutochukua hatua kwa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) pamoja na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) kuhusu uhalifu unaoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wa palestina .
Habari ID: 3481885    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/03

IQNA-Maelfu kwa maelfu ya watu wamejitokeza mitaani katika nchi kadhaa za Ulaya kushiriki maandamano ya kuunga mkono Palestina, huku wakiushutumu utawala dhalimu wa Israel kwa kukiuka mara kwa mara makubaliano ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza kati yake na Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas.
Habari ID: 3481878    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/01

IQNA –Afrika Kusini imemtangaza kaimu balozi wa utawala wa Isarel nchini humo kuwa mtu asiyehitajika na kuamuru afukuzwe mara moja.
Habari ID: 3481876    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/31

IQNA – Pep Guardiola kocha wa timu ya Ligi Kuu ya Soka Uingereza (EPL), Manchester City, ameeleza hadharani uungaji mkono wake kwa wananchi wa Palestina, akielekeza macho ya ulimwengu kwenye janga kubwa la kibinadamu linaloikumba Gaza, wakati wa tukio la hadhara lililofanyika hivi karibuni.
Habari ID: 3481871    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/30

IQNA – Mkutano wa Kwanza wa Umoja wa Ummah wa Kiislamu kwa Ajili ya Palestina uliofanyika Kuala Lumpur, Malaysia, umekamilisha shughuli zake kwa kutoa tamko la mwisho.
Habari ID: 3481844    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/25

IQNA – Umoja wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu (International Union of Muslim Scholars – IUMS) umetoa fatwa (hukumu ya kidini) ikitangaza kwamba kuwa na mahusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel ni haramu kisheria kwa mujibu wa Uislamu.
Habari ID: 3481830    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/21

IQNA – Katibu Mkuu wa Jukwaa la Kimataifa la Umoja na Kukurubisha Madhehebu ya Kiislamu (WFPIST) amesisitiza haja ya kuimarisha umoja na kudumisha umakini wa ulimwengu wa Kiislamu kuhusu suala la Palestina.
Habari ID: 3481825    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/20

IQNA – Maelfu ya waandamanaji walijitokeza Ijumaa katika mji mkuu wa Morocco kupinga hatua ya nchi hiyo ya kuendeleza uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3481788    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/11

IQNA – Wapigania haki za Wa palestina wamezindua kampeni mahsusi ya vyombo vya habari yenye lengo la kuwakomboa wafungwa walioko katika magereza ya utawala wa Kizayuni wa Israel, wakisisitiza kuwa mshikamano wa kimataifa na uelewa mpana ndiyo nguzo kuu ya kufanikisha uhuru wao.
Habari ID: 3481783    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/08

Amri ya hivi karibuni ya utawala wa  Israel, iliyondoa mamlaka ya manispaa ya al-Khalil (Hebron) katika maamuzi ya mipango kuhusu eneo nyeti la msikiti huo, inaendelea kukosolewa vikali.
Habari ID: 3481752    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/02

IQNA – Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi wa Ki palestina ameonya kwamba vizuizi vipya vilivyowekwa na Israel vinakwamisha kabisa usambazaji wa misaada huko Gaza, vinazidisha hali ya njaa na kuweka “mfano hatari” kwa shughuli za kibinadamu duniani kote.
Habari ID: 3481749    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/01

IQNA-Wakipita njia zilizozungukwa na majengo yaliyoharibiwa na vifusi, wanafunzi Wa palestina wa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Gaza wiki hii wamerudi darasani kwa mara ya kwanza baada ya miaka miwili.
Habari ID: 3481692    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/21