palestina

IQNA

IQNA – Hafla maalumu imeandaliwa kwa ajili ya kuwatunuku zawadi na kuwaenzi vijana 600 waliohifadhi Qur’ani Tukufu katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3482530   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/24

IQNA – Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, amemtaja Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kuwa ni mhalifu wa kivita, na kuitaka serikali ya Marekani kutekeleza hati ya kukamatwa kwake iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) iwapo atatia mguu katika ardhi ya Marekani.
Habari ID: 3482524   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/22

IQNA – Magenge ya walowezi wa Kizayuni yamefanya mfululizo wa mashambulizi ya kikatili usiku wa Jumapili katika miji na vijiji mbalimbali katika wilaya za al-Khalil (Hebron) na Nablus katika eneo linalokaliw akwa mabavu na Israel la Ukingo wa Magharibi, ambapo wamechoma moto nyumba na msikiti, wamewashambulia wakazi, na kupora mifugo huku wakilindwa na wanajeshi wa utawala katili wa Israel.
Habari ID: 3482514   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/20

IQNA-Afisa mwandamizi wa Harakati ya Kiislamu ya Mapambano ya Palestina, Hamas, ametoa pongezi za dhati kwa Uhispania kufuatia ushindi wake baada ya mechi ngumu katika fainali ya Kombe la Dunia la FIFA la mwaka 2026, akielezea mafanikio hayo kuwa ni chanzo cha furaha kwa watu wa Palestina na wafuasi wote wa haki, huku akibainisha kuwa ushindi huo ni pigo hasa kwa utawala wa Kizayuni wa Israel na wafadhili wake.
Habari ID: 3482512   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/20

IQNA – Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, amesema Jumamosi kuwa utawala wake unachunguza iwapo una mamlaka ya kisheria ya kumkamata Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel, Benjamin Netanyahu, iwapo atatembelea jiji hilo kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwezi Septemba.
Habari ID: 3482506   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/19

IQNA – Mtaalamu Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Ardhi za Palestina Zinazokaliwa kwa Mabavu, Francesca Albanese, ametoa wito siku ya Jumapili kwa hati ya haraka ya kukamatwa kwa Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni, Yisrael Katz, baada ya waziri huyo kukiri kufanya jinai za kivita huko Gaza na Lebanon.
Habari ID: 3482478   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/13

IQNA – Mashindano ya Kombe la Dunia la 2026 yanafanyika kote Amerika Kaskazini, lakini “sauti” kuu ya michuano hiyo inayoimbwa bila shaka ni ile ya kuunga mkono Palestina.
Habari ID: 3482439   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/04

IQNA – Mahmoud Khalil, mwanaharakati Mpalestina, amekata rufaa katika Mahakama Kuu ya Marekani ili kuzuia kufukuzwa kwake nchini humo.
Habari ID: 3482279   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/24

IQNA – Kuanzia Gaza hadi Catalonia, Pep Guardiola amedhihirisha kuwa anaamini mambo makubwa zaidi ya soka. Kocha huyo wa Manchester City amejipatia sifa duniani kama mmoja wa watu mashuhuri wanaosimama kidete kutetea haki za watu wa Palestina.
Habari ID: 3482274   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/23

IQNA – Watetezi wa haki za binadamu na maafisa wa Palestina wameilaani hatua wanayoieleza kuwa ni kukiuka kwa mfumo uhuru wa ibada, baada ya utawala haramu wa Israel kwa mara nyingine kuzuia maelfu ya Wapalestina wa Gaza kusafiri kwenda Saudi Arabia kwa ajili ya Hija ya kila mwaka.
Habari ID: 3482268   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/22

IQNA – Mchezaji wa Ufaransa, Sacha Bouy, alivutia hisia wakati wa sherehe za ubingwa wa Ligi ya Uturuki za klabu yake Galatasaray, alipohudhuria hafla ya kukabidhiwa kombe akiwa amebeba bendera ya Palestina.
Habari ID: 3482254   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/18

IQNA – Mlipuko mkubwa umetokea katika kituo cha viwanda katika eneo la Beit Shemesh karibu na mji mtakatifu wa Al‑Quds (Jerusalem), huku mtikisiko wake ukihisiwa katika maeneo mbalimbali ya ardhi zinazokaliwa kwa mabavu ambazo zimepachikwa jina la 'Israel'.
Habari ID: 3482248   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/17

Maafisa wa UN katika Siku ya Ukumbusho wa Nakba
IQNA – Wakikumbuka mwaka wa Nakba Ijumaa, maafisa wakuu wa Umoja wa Mataifa wameonya kwamba mateso na uhamishaji walioupata Wapalestina tangu mwaka 1948, baada ya ardhi yao kukoliniwa na Israel, ni maumivu yanayoendelea kwa vizazi na maelfu ya kilomita.
Habari ID: 3482243   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/16

IQNA – Uamuzi wa nyota wa soka wa Hispania, Lamine Yamal, kupeperusha bendera ya Palestina wakati wa gwaride la ushindi wa Barcelona katika La Liga umeibua wimbi kubwa la uungwaji mkono duniani.
Habari ID: 3482237   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/13

IQNA – Katika kumbukumbu ya tukio lenye kuhuzunisha, shirika la Amnesty International limeilaani vikali utawala wa Israel kwa kuendelea kumshikilia daktari wa Gaza, Dkt. Hussam Abu Safiya.
Habari ID: 3482229   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/12

IQNA – Msafara wa meli unaojulikana kama Global Sumud Flotilla, unaolenga kuvunja mzingiro uliowekwa na utawala katili wa Israeli dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, umefika katika maji ya kimataifa karibu na pwani ya Ugiriki.
Habari ID: 3482179   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29

IQNA – Sheikh Raed Salah na Sheikh Kamal al‑Khatib wamelaani marufuku ya wiki moja iliyowekwa na mamlaka za utawala haramu wa Israel kuwazuia kuingia katika Msikiti wa Al‑Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala huo, wakisema ni “shambulio dhidi ya dini yetu.”
Habari ID: 3482178   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29

IQNA – Wakielezea kama uhamasishaji mkubwa zaidi wa aina yake, wanaharakati wa kimataifa wametangaza mipango ya kupeleka meli 200 katika msafara wa misaada unaojulikana kama Freedom and Sumud Flotilla, wakilenga Ukanda wa Gaza katika majira ya kuchipua mwaka huu.
Habari ID: 3482002   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/27

IQNA — Wizara ya Awqaf na Masuala ya Kiislamu ya Palestina imetangaza mpango jumuishi wa kuukaribisha na kuadhimisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika Msikiti wa Al‑Aqsa, uliopo katika mji mtakatifu wa al‑Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na Israel.
Habari ID: 3481954   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/18

IQNA-Kiongozi wa harakati ya Muqawama (mapambano ya Kiislamu) ya Ansarullah nchini Yemen amesema kuwa Marekani na Utawala wa Israel zinakabiliana na Iran kwa sababu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasimama kama kizuizi dhidi ya mradi wao mpana wa kutawala eneo la Asia Magharibi au Mashariki ya Kati.
Habari ID: 3481932   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/14