IQNA

Picha: Hafla ya Kiheshima ya Kufuta Vumbi Yafanyika katika Haram Takatifu ya Imam Ridha (AS) Kabla ya Wiki ya Karamat

IQNA – Katika mkesha wa kuadhimisha Wiki ya Karamat na kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Hadhrat Masoumah (SA), sherehe ya kifakhari ya kufuta vumbi ilifanyika katika haram takatifu ya Imam Ridha (AS) mjini Mashhad, mnamo tarehe 28 Aprili 2025.

Tukio hilo lilihudhuriwa na mfawidhi wa Idara ya Haram ya Imam Ridha (AS) ambayo inajulikana kama Astan Quds Razavi , pamoja na kundi la wanazuoni, familia za mashujaa waliouawa shahidi, wasanii, watumishi wa haram, na wananchi wa kawaida.

Wiki ya Karamat huadhimisha siku za kuzaliwa kwa Hazrat Masoumah (SA) na Imam Ridha (AS), ambazo mwaka huu zinaangukia tarehe 29 Aprili na 9 Mei, mtawalia. Ni kipindi cha Ziyara katika maeneo hayo mawili matakatifu, sherehe, na matukio ya kitamaduni, hasa katika miji kama Mashhad na Qom.

 

 

Chanzo za picha:razavi.ir

Kishikizo: imam ridha as ، MASOUMA